Posted by On the spot Tz
2:33:00 AM
0
Donald Trump, anayewania kuteuliwa na chama chake cha Republican kugombea urais wa Marekani na ambaye ni maarufu kwa maneno ya chuki dhidi ya Waislamu, hivi sasa anaonekana kuhaha kutafuta kura za Waislamu.
Gazeti la The Hill linaloandika sana habari za Baraza la Congress la Marekani limeripoti kuwa, Walid Phares, mshauri wa masuala ya usalama wa taifa wa Donald Trump amekuwa akitumia kimya cha vyombo vya habari kuzungumza na kujaribu kuwashawishi Waislamu wanachama wa chama cha Republican pamoja na wanaharakati wahafidhina wenye asili ya Mashariki ya Kati nchini Marekani wamuunge mkono Donald Trump.
Juhudi za siri za timu ya uchaguzi ya Trump za kusaka kura za Waislamu zinafanyika katika hali ambayo mara kwa mara Donald Trump amekuwa akilaumiwa vikali kutokana na matamshi yake ya chuki dhidi ya Waislamu.
Miongoni mwa matamshi ya chuki dhidi ya Waislamu yaliyotolewa na mwanasiasa huyo wa Marekani ni kutaka Waislamu wazuiwe kuingia Marekani na vile vile kitendo chake cha kutaka kuanzishwe kitengo maalumu cha kuwafanyia ujasusi Waislamu nchini humo.

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: