Posted by On the spot Tz
3:57:00 AM
0
Straika wa Mwadui FC, Jerry Tegete, amelishukia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) akidai hajui hatma ya malipo ya fedha anazoidai Yanga baada ya malalamiko yake kufika kwenye shirikisho hilo.
Tegete anaidai Yanga Sh milioni 10, ikiwa ni malipo yake ya kuvunjiwa mkataba msimu wa 2014/2015 kabla ya kutimkia Mwadui.
Tegete alisema suala lipo mezani kwa Kamati ya Nidhamu ya TFF iliyokutana Julai 3, 2016 na kujadili masuala mbalimbali likiwemo la Geita Gold, lakini anashangaa limewekwa pembeni na kutojadiliwa.
Tegete alisema, mara baada ya suala lake kutojadiliwa, alimtafuta Mkurugenzi Msaidizi wa Sheria na Uanachama wa TFF, Eliud Peter Mvela lakini hakumpa majibu sahihi juu ya madai yake.
“Ninavyosikia Yanga kwa kushirikiana na mmoja wa viongozi wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, wamepanga kutudhulumu mimi na wengine tunaowadai, kiukweli sitakubali kuona haki yangu inapotea.
“Yanga tayari wamenilipa Sh milioni 10 na imebakia Sh milioni 10 baada ya kuvunja mkataba wangu wa mwaka mmoja uliobaki kuichezea Yanga, naomba Malinzi (Rais wa TFF, Jamal) anisaidie nilipwe,” alisema Tegete.
Alipotafutwa Mvela kuzungumzia hilo simu yake ya mkononi haikupatikana, lakini Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa akizungumzia suala hilo alisema: “Ngumu kulizungumzia hilo, kwani halipo kwenye meza yangu.”
Sh Mil 20
Jumla ya fedha
za madai ya Tegete kwa Yanga

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: