Posted by On the spot Tz
3:55:00 AM
0

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema hatakuwa tayari kupokea ofa ya Klabu ya Golden Arrows ya Afrika Kusini kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wao, Ibrahim Ajib.
Poppe amesema hayo huku kukiwa na taarifa kuwa, Ajib amefuzu majaribio yake katika Klabu ya Golden Arrows na kilichobaki ni timu hizo kukubaliana kuhusu usajili tu.
Poppe alionyesha kukerwa na kitendo cha Ajib kuondoka Simba bila ya kuaga kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio Golden Arrows inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini.
Ajib aliondoka nchini na anayetambulika kama meneja wake, Juma Ndambile huku kukiwa na sintofahamu ya mkataba wake, mwenyewe alidai umeisha lakini Simba wanakataa.
“Hiyo ofa binafsi siihitaji, wanaweza kuijadili na wakala wake kama alivyoondoka hapa. Hii maana yake ni sawa na mtu amejaribu kukuibia halafu kashindwa, sasa anakuja kukuomba umpe alichohitaji, siyo sawa.
“Hatujui tumchukulie hatua gani Ajib lakini tukishakaa na kujadili tutajua inakuwaje kuhusiana na masuala yake yote. Lakini najaribu kumuangalia hata huyu meneja wake, anafahamika kuwa ni mtu wa Simba na kuna kipindi aliwahi kupewa cheo.
"Sasa inakuwaje anadanganywa na mchezaji naye anakubali tu? “Alishindwa nini kuja kuhakikisha kuhusu mkataba wa Ajib mpaka akaamua kuchukua uamuzi wa kuondoka naye bila ruhusa? Na hao Golden Arrows inakuwaje wanazungumza na mchezaji mwenye mkataba kamili timu nyingine?” alihoji Hans Poppe.
Alisema moja kati ya hatua watakazochukua ni kuandika barua Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Chama cha Soka Afrika Kusini (Safa) kuhusu kitendo cha meneja huyo, Ajib na Golden Arrows kuwasiliana bila ruhusa ya Simba.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: