Posted by On the spot Tz
4:04:00 AM
0
Na Tom
Machupa kutoka Tanga,
Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Tanga BENEDICT WAKULYAMBA.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Tanga BENEDICT WAKULYAMBA amesema Jeshi la Polisi mkoani hapo
linaendelea na oparesheni ya kukamata waendesha piki piki maarufu kama BODA BODA wasiovaa au kuwavalisha abiria wao kofia ngumu
(HELMENT) wakati wakiwa katika safari
zao mbalimbali lengo ni kuepusha vifo
visivyo vya lazima kutokana na madereva hao kutokutii sheria za usalama
barabarani.
Mwendesha Boda Boda anayevunja sheria za usalama barabarani.
Kamanda
WAKULYAMBA amesema jukumu la kuvaa kofia
ngumu si la dereva pekee bali hata abiria anatakiwa kuvaa kofia ngumu ili awe na usalama wakati wote ambao anatumia usafiri wa aina hio, Kwa yeyote
ambaye hata heshimu sheria za Usalama Barabarani jeshi la polisi litamchukulia hatua kwa
mujibu wa sheria za usalama barabarani.
Aidha
kamanda WAKULYAMBA amesema mpaka sasa Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa
thelathini (30) ambao wamekaidi maagizo na kuvunja sheria za barabarani ikiwemo kutokuvaa kofia ngumu (HELMENT)
wakiwemo madereva wa pikipiki (BODA BODA)
na abiria wao.
Mwendesha boda boda na Abiria wake wakiwa wamevaa kofia ngumu (HELMENT)
Kamanda WAKULYAMBA
amewaomba wananchi wa Tanga kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la
polisi wanapohisi au kupata taarifa zozote za kihalifu ili Jeshi la polisi
liweze kushughulikia ili Nchi na Mkoa kuwe na amani kwa ujumla.
Waendesha Boda boda wakiwa katika eneo lao la kazi.
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Kijana Shoga Amtia Doa Mwanamuziki Raymond wa wasafi, Adai Wana Mahusiano,,,,,,,,,,,,,Leo katika kuperuzi kwenye mitandao ya kijamii nimekutana na post za kijana wa kiume ambazo zinamuhusu msanii Raymond wa wasafi,post za k...




No comments: