Posted by On the spot Tz
2:49:00 AM
0
Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa kuonesha ligi ya Bundesliga kwa msimu wa mwaka 2017/18 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kampuni ya Startimes Tanzania imezindua uoneshaji wa ligi ya Bundesliga mwaka 2017/2018 ambayo itarushwa mubashara kupitia vipindi vya startimes kwa wapenzi wa soka hapa nchini
Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam lengo ni kuwa kuwafahamisha wapenzi wa mpira kununua ving’amuzi na kujiunga na vifurushi ili kuburudika na mechi hizo ambazo ligi hiyo itakuwa ikiionyeshwa moja kwa moja na startimes.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif amesema kuwa ipo fursa kwa waandishi wa habari za michezo kufanya mashindano ya uandishi wa mechi hiyo na kwa mshindi wa shindano hilo atagharamiwa safari zote za ti ya ndege kwenda moja kwa moja Ujerumani.
Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa StarTimes Tanzania, Juma Suluhu nae amesema wana mahusiano mazuri na bundesliga kwa kuwa na mkataba wa miaka mitano na hadi sasa ni mwaka wa tatu kuonyesha ligi hiyo.
Meneja Uwendeshaji Startimes, Gaspa Ngowi amesema kuwa huduma mpya ya malipo kwa wale wenye hali ya chini wanaweza kulipia siku moja king’amuzi cha Startimes kwa gharama ya bei ya shilingi 1000, ambapo kwa wiki utalipia elfu 4000.
Hata hivyo mhariri mkuu wa gazeti la Championi , Salehe Jembe amesema kuwa ligi ya Bundesliga ina ubora na kuburudisha zaidi kulinga na ligi zingine duniani kwa kuwa na wachezaji bora
Nae Meneja mahusiano wa Tabibu TV, Kaki Mwaigomole ametoa shukrani kwa kampuni ya startimes kwa kuwapa fursa ya kuweza kuonyesha mubashara mtanange huo ambao utaanza rasmi tarehe 18-27 Agosti mwaka huu
Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif(wa pili kutoka kushoto) akikata utepe pamoja na wadau mbalimbali wa mpira hapa nchini.
Baadhi ya wafanyakazi wa StarTimes Tanzania wakfuatilia yaliyokuwa yanajiri kwenye uzinduzi huo
Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa StarTimes Tanzania, Juma Suluhu akizungumza kuhusu kampuni hiyo wanavyoshirikiana kuonesha ligi ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga
Picha ya Pamoja .

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel. «
Next
This is the most recent post.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: