
Posted by On the spot Tz
6:08:00 AM
0
Na Tom Machupa kutoka Tanga,
Meneja wa kiwanda cha Tanga Fresh MICHAEL KARATA akionyesha hati waliopokea kutokana na agizo la mhe.Rais mbele ya waandishi wa habari.
Agizo
la Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI
alilolitoa siku ya jumapili tarehe
6/8/2017 wakati alipotembelea kiwanda cha kuzalisha maziwa mkoani Tanga
kijulikanacho kwa jina la Tanga Fresh kuhusu kuachiliwa kwa hati ya umiliki wa
Ardhi ya kiwanda hicho ambayo ilizuiliwa
tangu mwaka 2011 limetekelezwa ikiwa ni siku ni siku tatu (3) tangu agizo hilo
lilipo tolewa.
Akizungumza
kwaniaba ya uongozi
wa Tanga freshi meneja mkuu Michael Karata amesema wanamshukuru mhe.Rais Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI kwakukubali ombi lao
ambalo lilikuwa kikwazo cha kutoendeleza uzalishaji wa kiwanda hicho. Pia meneja Karata
amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela kwakumshawishi Raisi Magufuli
kutembelea kiwanda chao kwani imewapa hamasa kubwa na motisha ya kufanya kazi kwa bidii.
Meneja mkuu wa Tanga fresh MICHAEL KARATA.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa bodi ya
wafugaji katika kiwanda cha Tanga fresh Hassan Mzee amesema wao kama wafugaji
wanakila sababu ya kuhakikisha wanazalisha maziwa kwa wingi ili kukifanya
kiwanda hicho kufanya kazi zake kwa ufanisi na kuwahudumia watu wengi zaidi
kuliko hivi sasa.
Makamu mwenyekiti wa bodi ya wafugaji Hassan Mzee.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela hakusita kumshukuru Rais Magufuli kwa
kuonyesha upendo wake kwa wananchi wa Tanga na kwakitendo cha kutatua matatizo
yao kwa haraka pasipo kuchelewa,Aidha
mkuu wa mkoa martin shigela ameuomba Uongozi wa kiwanda cha Tanga Fresh
kutumia hati hio kwa mipango waliojipangia tangu awali ili kuenenda sawa na nia ya Rais katika
kutengeneza Tanzania ya viwanda.
Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela Akiongea mbele ya waandishi wa habari.
Mkuu
wa Mkoa pia ametumia nafasi hio kuwaambia wanahabari kuwa maagizo yote aliyotoa
Rais Magufuli yatafanyiwa kazi kwa haraka na ufanisi mkubwa kwa kufwata sharia na
kanuni za nchi bila kumpendelea mtu yoyote.
Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa kiwanda cha Tanga Fresh.

Tagged with:
HABARI KITAIFA

On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
- quantalfaggart says:
Best Casinos in Las Vegas, NV - Mapyro
The best casinos in Las... more
Pageviews
64,455
No comments: