
Posted by On the spot Tz
7:31:00 AM
0
Katika kile kinachoonekana sasa presha imeanza kuwa kubwa kwa mabosi wa Ligi Kuu Bara kuhusu ubingwa, licha ya kuwa bado ni hatua za mwanzoni katika msimu wa 2016/17 tayari kumekuwa na tambo kila kona huku timu kubwa za Simba na Yanga zikianza kutupiana vijembe.
Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm amewaambia wapinzani wake, Simba kuwa wanajidanganya kuufikiria ubingwa wa ligi hiyo kwa kuwa bado ni mapema.
Pluijm ametoa kauli hiyo mara baada ya mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Simba na Yanga kumalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga inashika nafasi ya tano ikiwa na pointi 11 katika michezo sita huku Simba ikiwa inaongoza ligi ikiwa na pointi 17 katika mechi saba.
Pluijm amesema itakuwa ajabu Yanga kuondolewa kwenye mbio za ubingwa wakiwa wamecheza mechi sita tu.
"Kama wanajipa matumaini hayo ya ubingwa, basi watakuwa wanajidanganya, tungojee ligi imalizike halafu uone hao Simba kama watakuwa mabingwa," alisema Pluijm.
Wakati huohuo, Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, amefunguka kuwa, mpaka sasa bado hajaona timu ambayo itakuja kuisumbua timu yake katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
“Najua si rahisi kuendelea kung’ang’ania kileleni wakati kuna mechi nyingi zimebaki, lakini hilo halitutishi sana, tutapambana iwe nyumbani au ugenini, ni lazima tupate pointi,” alisema Omog.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.

On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.You May Also Like
Usikose Bundesliga msimu wa tatu ndani ya startimes.
FULL TIME : Simba 1 - 0 Rayon sports katika mchezo wa Simba Day.
DK 45 : Zimemalizika Simba 1 - 0 Rayon sports.
LWANDAMINA AJIUZULU RASMI ZESCO SASA MKUU PANDE MKUU SAWA NDANI YA YANGA SC,,,,,,,,,,,,,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
- quantalfaggart says:
Best Casinos in Las Vegas, NV - Mapyro
The best casinos in Las... more
Pageviews
66,165
No comments: