Posted by On the spot Tz
7:31:00 AM
0
Katika kile kinachoonekana sasa presha imeanza kuwa kubwa kwa mabosi wa Ligi Kuu Bara kuhusu ubingwa, licha ya kuwa bado ni hatua za mwanzoni katika msimu wa 2016/17 tayari kumekuwa na tambo kila kona huku timu kubwa za Simba na Yanga zikianza kutupiana vijembe.
Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm amewaambia wapinzani wake, Simba kuwa wanajidanganya kuufikiria ubingwa wa ligi hiyo kwa kuwa bado ni mapema.
Pluijm ametoa kauli hiyo mara baada ya mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Simba na Yanga kumalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga inashika nafasi ya tano ikiwa na pointi 11 katika michezo sita huku Simba ikiwa inaongoza ligi ikiwa na pointi 17 katika mechi saba.
Pluijm amesema itakuwa ajabu Yanga kuondolewa kwenye mbio za ubingwa wakiwa wamecheza mechi sita tu.
"Kama wanajipa matumaini hayo ya ubingwa, basi watakuwa wanajidanganya, tungojee ligi imalizike halafu uone hao Simba kama watakuwa mabingwa," alisema Pluijm.
Wakati huohuo, Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, amefunguka kuwa, mpaka sasa bado hajaona timu ambayo itakuja kuisumbua timu yake katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
“Najua si rahisi kuendelea kung’ang’ania kileleni wakati kuna mechi nyingi zimebaki, lakini hilo halitutishi sana, tutapambana iwe nyumbani au ugenini, ni lazima tupate pointi,” alisema Omog.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: