

Posted by On the spot Tz
9:22:00 PM
0
Wasanii wanne wa kundi la vichekesho la Orijino Komedi akiwamo meneja wao wamekamatwa na kuhojiwa na jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kosa la kuwa na sare za polisi.
Juzi, jeshi hilo lilitoa onyo kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama nchini na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria.
Kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni za Makosa ya Jinai, sura ya 16 na marejeo yake ya mwaka 2002, kifungu cha 178 (1) na (2) kinachozungumzia makosa dhidi ya sare za majeshi ya ulinzi na usalama, kinabainisha kuwa ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ambaye siyo mtumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama kuvaa mavazi yanayotumiwa au kushabihiana na sare za majeshi hayo bila kibali kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kaimu Kamanda wa Kanda hiyo, Hezron Gyimbi alisema wasanii hao walikamatwa juzi saa 10 jioni baada ya kusambaa kwa video kwenye mitandao ya kijamii wakiwa wamevalia sare hizo kwenye sherehe ya harusi ya Emmanuel Mgaya maarufu ‘Masanja’.
Gyimbi aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Lucas Lazaro (Joti), Alex John (McRegan) na Isaya Gidion (Wakuvanga) na Sekioni David (Seki) ambaye ni meneja wao.
Alisema sare walizokutwa nazo watuhumiwa hao ni za kazi za kawaida za jeshi la polisi hilo ikiwamo kofia, filimbi, shati, suruali, cheo na mkanda.
“Tunaendelea kuwachunguza zaidi kama wana vitu vingine vya jeshi la polisi na tunataka kujua kuwa sare hizi wamepa- ta kibali kwa nani na uhalali wa kuwa nazo,” alisema Gyimbi.
Alisema jeshi hilo linaendelea kumtafuta Masanja ili kujibu tuhuma zinazomkabili. Kaimu kamanda huyo alisema watuhumiwa hao walihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi kuanzia juzi saa 10 jioni hadi jana jioni huku na dhamana zao zilikuwa wazi.
Juzi, jeshi hilo lilitoa onyo kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama nchini na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria.
Kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni za Makosa ya Jinai, sura ya 16 na marejeo yake ya mwaka 2002, kifungu cha 178 (1) na (2) kinachozungumzia makosa dhidi ya sare za majeshi ya ulinzi na usalama, kinabainisha kuwa ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ambaye siyo mtumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama kuvaa mavazi yanayotumiwa au kushabihiana na sare za majeshi hayo bila kibali kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kaimu Kamanda wa Kanda hiyo, Hezron Gyimbi alisema wasanii hao walikamatwa juzi saa 10 jioni baada ya kusambaa kwa video kwenye mitandao ya kijamii wakiwa wamevalia sare hizo kwenye sherehe ya harusi ya Emmanuel Mgaya maarufu ‘Masanja’.
Gyimbi aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Lucas Lazaro (Joti), Alex John (McRegan) na Isaya Gidion (Wakuvanga) na Sekioni David (Seki) ambaye ni meneja wao.
Alisema sare walizokutwa nazo watuhumiwa hao ni za kazi za kawaida za jeshi la polisi hilo ikiwamo kofia, filimbi, shati, suruali, cheo na mkanda.
“Tunaendelea kuwachunguza zaidi kama wana vitu vingine vya jeshi la polisi na tunataka kujua kuwa sare hizi wamepa- ta kibali kwa nani na uhalali wa kuwa nazo,” alisema Gyimbi.
Alisema jeshi hilo linaendelea kumtafuta Masanja ili kujibu tuhuma zinazomkabili. Kaimu kamanda huyo alisema watuhumiwa hao walihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi kuanzia juzi saa 10 jioni hadi jana jioni huku na dhamana zao zilikuwa wazi.

Tagged with:
Burudani

On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.You May Also Like
Utalipenda jibu la Martin Kadinda baada ya kuulizwa na shabiki kama Wema anatumia Madawa ya kulevya,,,,,,,,,,,
AUDIO: Sikiliza Bifu la Wema Sepetu na Man Fongo...Mama Wema Atoa Mapovu,,,,,,,,,,,
Wema: Nitalipa Pesa Matibabu ya Baba diamond,,,,,,,,,,,,,,,,,
Kijana Shoga Amtia Doa Mwanamuziki Raymond wa wasafi, Adai Wana Mahusiano,,,,,,,,,,,,,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
- quantalfaggart says:
Best Casinos in Las Vegas, NV - Mapyro
The best casinos in Las... more
Pageviews
65,866
No comments: