Posted by On the spot Tz
9:24:00 AM
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani kimeanza kugawa vifaa zikiwemo bendera kwa ajili maandalazi ya Umoja wa Kupinga Udikteta ( Ukuta) ambayo yanatarajia kufanyika Septemba mosi mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Kanda ya Pwani wa Chadema, Casimir Mabina, alisema kuwa bendera hizo zitaanza kupeperushwa kuanzia kesho kutwa kwa ajili ya kuunga mkono azimio la Kamati Kuu ya kufanyika oparesheni Ukuta.
Alisema oparesheni Ukuta ni lazima ifanyike nchi nzima na kwamba hawako tayari kuona ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya tano ambayo imeonyesha viashiria vya utawala wa kidikteta.
Alisema Rais John Magufuli, anajaribu kuua demokrasia ya vyama vingi kwa kukataza na kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani huku CCM ikiendelea na mikutano yake kama kawaida.
“Tumeona jinsi Rais alivyopiga marufuku wapinzani kukutana kwenye mikutano ya hadhara huku akiwatishia kuwa wakikaidi atawashughulikia na kweli amewaamuru polisi watekeleze amri hiyo ya kuwakamata viongozi wa Chadema na kuwafungulia mashtaka,” alisema
Aliongezea kuwa mbaya zaidi Jeshi la Polisi linazuia hata mikutano ya ndani ya vyama vya upinzani na makongamano na hata mahafali ya wanafunzi wenye itikadi za upinzani licha ya kutambua kuwa mikutano ya ndani haiwezi kuleta uvunjifu wa amani kwa walio ndani ya ukumbi.
Alisema licha ya kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli. amekataza mikutano hiyo kufanyika chama tawala, kinafanya mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali kwa kisingizio cha shughuli za serikali.
Mabina alisema juzi CCM ilisema itakuwa na maandamano kutoka uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere ya kumpokea Rais Magufuli hadi Makao Makuu ya CCM yaliyopo Lumumba.
“Tunahoji haki ya kufanya siasa ni kwa CCM tu na siyo kwa vyama vingine? Hili jambo hatuwezi kukubali Jeshi la Polisi lituambie inakuwaje vibali vinatolewa kwa CCM halafu upinzani tunyimwe tunasema lazima tufanye oparesheni Ukuta ya kupinga ukandamizaji wa demokrasia,” alisema Mabina
Naye Katibu wa Wabunge wa Upinzani Mkoa wa Dar es Salaam, Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Theonest, alisema lengo la oparesheni ya Ukuta ni kupinga ukandamizaji unaofanywa na serikali.
Alisema wana haki ya kikatiba ya kufanya mikutano bila kuzuiliwa kama ambayo wamefanyiwa na ndio maana wameanza kugawa bendera kwa ajili ya kujiandaa na oparesheni hiyo.
onthespottz.blogspot.com
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Kanda ya Pwani wa Chadema, Casimir Mabina, alisema kuwa bendera hizo zitaanza kupeperushwa kuanzia kesho kutwa kwa ajili ya kuunga mkono azimio la Kamati Kuu ya kufanyika oparesheni Ukuta.
Alisema oparesheni Ukuta ni lazima ifanyike nchi nzima na kwamba hawako tayari kuona ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya tano ambayo imeonyesha viashiria vya utawala wa kidikteta.
Alisema Rais John Magufuli, anajaribu kuua demokrasia ya vyama vingi kwa kukataza na kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani huku CCM ikiendelea na mikutano yake kama kawaida.
“Tumeona jinsi Rais alivyopiga marufuku wapinzani kukutana kwenye mikutano ya hadhara huku akiwatishia kuwa wakikaidi atawashughulikia na kweli amewaamuru polisi watekeleze amri hiyo ya kuwakamata viongozi wa Chadema na kuwafungulia mashtaka,” alisema
Aliongezea kuwa mbaya zaidi Jeshi la Polisi linazuia hata mikutano ya ndani ya vyama vya upinzani na makongamano na hata mahafali ya wanafunzi wenye itikadi za upinzani licha ya kutambua kuwa mikutano ya ndani haiwezi kuleta uvunjifu wa amani kwa walio ndani ya ukumbi.
Alisema licha ya kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli. amekataza mikutano hiyo kufanyika chama tawala, kinafanya mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali kwa kisingizio cha shughuli za serikali.
Mabina alisema juzi CCM ilisema itakuwa na maandamano kutoka uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere ya kumpokea Rais Magufuli hadi Makao Makuu ya CCM yaliyopo Lumumba.
“Tunahoji haki ya kufanya siasa ni kwa CCM tu na siyo kwa vyama vingine? Hili jambo hatuwezi kukubali Jeshi la Polisi lituambie inakuwaje vibali vinatolewa kwa CCM halafu upinzani tunyimwe tunasema lazima tufanye oparesheni Ukuta ya kupinga ukandamizaji wa demokrasia,” alisema Mabina
Naye Katibu wa Wabunge wa Upinzani Mkoa wa Dar es Salaam, Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Theonest, alisema lengo la oparesheni ya Ukuta ni kupinga ukandamizaji unaofanywa na serikali.
Alisema wana haki ya kikatiba ya kufanya mikutano bila kuzuiliwa kama ambayo wamefanyiwa na ndio maana wameanza kugawa bendera kwa ajili ya kujiandaa na oparesheni hiyo.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: