Posted by On the spot Tz
9:27:00 AM
0
PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amezomewa na wafanyabiashara wadogowadogo (wamachinga) mbele ya Rais John Magufuli, anaandika Faki Sosi.
Tukio hilo lilitokea jana katika ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizopo Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam baada ya Rais Magufuli kutoka mikoani kwa ziara yake ya kuwashukuru Watanzania.
Wafanyabiashara hao walifika kwenye ofisi hizo wakiwa na mabango yalio na maandishi yenye ujumbe wa malalamiko kwa rais dhidi ya Mgambo wa Jiji wanaowazuia kufanya biashara zao.
Wakati Rais Magufuli akizungumzia suala la mama lishe, wauza mbogamboga na wamachinga kuhusu kusumbuliwa na Mgambo wa Jiji, alisema ameteua viongozi wazuri akiwemo Makonda kama Mkuu wa Mkoa.
Lakini alipotajia jina la Makonda, sauti kutoka kwa wamachinga zilipiga kelele na kusema ‘jipu hilooooo baba,’ kelele hizo ziliendelea.
Rais Magufuli alisita kidogo kuongea kupisha zomea hiyo na baada ya muda mchache aliendelea kuzungumza.
Pamoja na Makonda kuzomewa, Rais Magufuli alisema, hataki kuona makundi hayo yakibaguliwa na kuagiza kuandaliwa kwa utaratibu mwingine.
Wamachinga hao walifika kwenye hadhara hiyo na mabango mbalimbali ambayo moja ya jumbe zilizoonekana kwenye mabango hayo ni pamoja na ‘Kilio chetu kwa Rais JPM ulituahidi ukiingia Ikulu mgambo watafute kazi nyengine…’ na ‘wamachinga tumekosa uhuru’ ambapo Rais Magufuli. Hata hivyo Rais Magufuli aliwataka watulie.
Kadhia ya kuzomewa Makonda mbele ya Rais Magufuli inamfika siku chache baada ya John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuzomewa mbele ya rais huyo.
Mongella alikumbana na kasheshe hiyo wakati akitoa taarifa fupi ya hali ya usalama na shughuli za maendeleo Mkoa wa Mwanza.
Akiendelea kusoma ghafla wananchi hao walianza kumzomea, hatua ya kuzomea ilianza pale Mongella alipodai kwambwa, hakuna njaa katika mkoa huo.
Mongella amedai kuwa, katika mkoa huo wa Mwanza, wamefanikiwa kuvuna chakula kingi na hakuna tatizo la njaa, kitendo ambacho kilipingwa na wananchi hao ambao walisikika wakidai, “acha uongo’ tuna njaa, hakuna chakula.”
onthespottz.blogspot.com
Tukio hilo lilitokea jana katika ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizopo Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam baada ya Rais Magufuli kutoka mikoani kwa ziara yake ya kuwashukuru Watanzania.
Wafanyabiashara hao walifika kwenye ofisi hizo wakiwa na mabango yalio na maandishi yenye ujumbe wa malalamiko kwa rais dhidi ya Mgambo wa Jiji wanaowazuia kufanya biashara zao.
Wakati Rais Magufuli akizungumzia suala la mama lishe, wauza mbogamboga na wamachinga kuhusu kusumbuliwa na Mgambo wa Jiji, alisema ameteua viongozi wazuri akiwemo Makonda kama Mkuu wa Mkoa.
Lakini alipotajia jina la Makonda, sauti kutoka kwa wamachinga zilipiga kelele na kusema ‘jipu hilooooo baba,’ kelele hizo ziliendelea.
Rais Magufuli alisita kidogo kuongea kupisha zomea hiyo na baada ya muda mchache aliendelea kuzungumza.
Pamoja na Makonda kuzomewa, Rais Magufuli alisema, hataki kuona makundi hayo yakibaguliwa na kuagiza kuandaliwa kwa utaratibu mwingine.
Wamachinga hao walifika kwenye hadhara hiyo na mabango mbalimbali ambayo moja ya jumbe zilizoonekana kwenye mabango hayo ni pamoja na ‘Kilio chetu kwa Rais JPM ulituahidi ukiingia Ikulu mgambo watafute kazi nyengine…’ na ‘wamachinga tumekosa uhuru’ ambapo Rais Magufuli. Hata hivyo Rais Magufuli aliwataka watulie.
Kadhia ya kuzomewa Makonda mbele ya Rais Magufuli inamfika siku chache baada ya John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuzomewa mbele ya rais huyo.
Mongella alikumbana na kasheshe hiyo wakati akitoa taarifa fupi ya hali ya usalama na shughuli za maendeleo Mkoa wa Mwanza.
Akiendelea kusoma ghafla wananchi hao walianza kumzomea, hatua ya kuzomea ilianza pale Mongella alipodai kwambwa, hakuna njaa katika mkoa huo.
Mongella amedai kuwa, katika mkoa huo wa Mwanza, wamefanikiwa kuvuna chakula kingi na hakuna tatizo la njaa, kitendo ambacho kilipingwa na wananchi hao ambao walisikika wakidai, “acha uongo’ tuna njaa, hakuna chakula.”
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: