Posted by On the spot Tz
2:50:00 AM
0
Kamandi ya jeshi la Lebanon imetangaza kunasa na kusambaratisha mfumo wa kijasusi wa utawala haramu wa Kizayuni katika miinuko ya al-Barouk nchini humo.
Taarifa iliyotolewa na jeshi hilo imeeleza kuwa, Jumanne ya jana askari wa nchi hiyo walifanikiwa kunasa vifaa hivyo katika miinuko ya mji huo wa al-Barouk na Ain Zhalta magharibi mwa nchi hiyo ambapo baada ya kuvinasa iliviharibu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, vifaa hivyo vya ujasusi ambavyo vilikuwa na mfumo wa kutuma picha na sauti, huku vikiwa na betri maalumu inayojichaji kila wakati, vinafanana na mawe ya eneo hilo suala ambalo ilikuwa vigumu kuvibaini. Kabla ya hapo Waziri wa Mawasiliano wa Lebanon, Boutros Harb alitangaza habari ya uepo wa mtandao wa ujasusi wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel nchini humo. Sanjari na kutaka kubaini mtandao huo, alitangaza kuwa timu ya kiutalaamu nchini Lebanon kwa kutumia vifaa vya kisasa vya upelelezi, ilifanikiwa kunasa mtandao huo. Ujasusi unaofanywa na utawala wa Kizayuni ni kati ya harakati za kiuadui zinazofanywa na utawala huo kwa ajili ya kupenyeza na kukiuka haki ya kujitawala taifa la Lebanon. Mbali na ujasusi, utawala huo wa Kizayuni umekuwa ukikiuka kujitawala kwa taifa hilo kupitia meli zake za kijeshi na ndege za kivita.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: