Posted by On the spot Tz
2:52:00 AM
0
Shirika la Kutetea Haki za Binaadamu la Human Rights Watch limewatuhumu askari wa kusimamia amani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kuwaua kiholela raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Taarifa iliyotolewa jana na shirika hilo imesema kuwa, askari hao wa Kongo DR ambao wanahudumu katika kikosi cha Umoja wa mataifa na Umoja wa Afrika (MINUSCA), waliwaua raia 18 wakiwamo wanawake na watoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati. Hata hivyo msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo sanjari na kukadhibisha madai hayo amesema kuwa, wizara hiyo imeanzisha uchunguzi kuhusiana na tuhuma hizo dhidi ya askari wake. Romin Oba ameongeza kuwa, serikali ya Kinshasa inashirikiana na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuwekwa wazi kadhia hiyo. Hii ni katika hali ambayo Stephan Dujarric, Msemaji wa Umoja wa Mataifa amenukuliwa akisema kuwa wafanyakazi wa Shirika la Kutetea Haki za Binaadamu la Human Rights Watch walizifanyia uchunguzi tuhuma hizo na kuwasilisha ripoti yao kwa viongozi wa kieneo. Ikiwa tuhuma hizo zitathibitishwa, basi zitawachafulia jina askari hao wa Kongo DR hasa kutokana na kuwa, kabla ya hapo pia askari wa nchi hiyo walituhumiwa kwa ubakaji na udhalilishaji wa kingono na kupelekea baadhi yao kurejeshwa nchini kwao.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: