Posted by On the spot Tz
2:31:00 AM
0
STEPHEN KESHI
MCHEZAJI na kocha wa zamani wa Nigeria, Stephen Okechukwu Keshi 'The Big Boss amefariki dunia mapema leo.
Keshi aliyefiwa na mkewe mwenye umri wa miaka 33, Kate, mwaka jana alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya saratani na inadhaniwa kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu huko jimbo la Benin Edo.
Kwa mujibu wa familia ya marehemu kocha huyo hakuonyesha dalili zozote za kuumwa kabla ya kifo chake. Ameacha watoto wanne na mama yake.
Keshi, kocha pekee Mnigeria kuiwezesha Super Eagles kushinda Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2013 na kuweka rekodi ya mtu wa pili barani kushinda taji hilo kama mchezaji na baadaye kocha.
Mtu mwingine aliyeweza kutwaa taji la AFCON kama mchezaji na baadaye kocha ni Mahmoud El-Gohary wa Misri.
Keshi aliichezea Nigeria kuanzia mwaka 1982 akiwa ana umri wa miaka 20 hadi mwaka 1994 na muda mrefu alikuwa Nahodha wa Super Eagles na alifunga mabao muhimu akiwa beki wa kati.
Pia amefundisha timu za taifa za Togo na Nigeria katika Kombe la Dunia pamoja na Mali. Mungu ampumzishe kwa amani gwiji wa soka Nigeria na Afrika.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: