Posted by On the spot Tz
8:27:00 AM
0

MBWANA SAMATA NA THOMAS ULIMENGU.
Sasa ni uhakika Tanzania haina nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kufungwa mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa.
Mohamed Salah anayekipiga AS Roma, ndiye aliyefunga mabao yote mawili akianza na lile la kipindi cha kwanza la mkwaju wa adhabu baada ya beki Haji Mwinyi kufanya madhambi.
Kipindi cha pili, Mwinyi tena alifanya kosa kwa kuzidiwa nguvu na Salah akapachika bao la pili akiwa amtulia kabisa.
Salah alifunga mabao yake katika dakika ya 44 na 58 na kuikatisha tamaa kabisa Stars na mashabiki wengi waliojitokeza kuishangilia timu yao ya taifa.
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alikosa penalti baada ya Himid Mao kuangushwa ndani ya enero la hatari.
Ushindi huo unaifanya Misri kufuzu baada ya kuwa imefikisha pointi 10, Nigeria iko katika nafasi ya pili ikiwa na pointi tatu na Tanzania inabaki mkiani na pointi moja.
Stars walicheza vizuri hasa kwa upande wa kumiliki mpira lakini tatizo likaonekana kutokuwa na mipango ya uhakika ili kujenga mbinu za kupata bao.
Stars walicheza vizuri hasa kwa upande wa kumiliki mpira lakini tatizo likaonekana kutokuwa na mipango ya uhakika ili kujenga mbinu za kupata bao.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: