Posted by On the spot Tz
2:25:00 AM
0
ZAKARIA HANS POPE.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ameondoka jana saa tatu na nusu usiku kwenda jijini Harare, Zimbabwe kumalizana na Kocha Kalisto Pasuwa.
Hans Poppe ameondoka na Ndege ya Shirika la Ndege la Fast Jet kwenda kukamilisha ‘Wanachotaka Wanasimba’.
Pasuwa sasa anakinoa kikosi cha timu ya taifa ya Zimbabwe na Simba ilifanya naye mazungumzo ya awali kwa simu na taarifa zinaeleza yuko tayari kutua Msimbazi.
Pamoja na Pasuwa, tayari Simba imefanya mazungumzo na mshambuliaji Mzimbabwe ambaye imeendelea kumficha.
Hans Poppe amezungumza na SALEHJEMBE na kusema anakwenda Zimbabwe kwa mambo yake ya kikazi.
“Kweli ninakwenda kwa masuala yangu ya kikazi, lakini kama kutakuwa na nafasi kwani shida ni nini kuzungumza nao?” alihoji Hans Poppe.
Hans Poppe alisema Simba inaendelea kujiimarisha kwa kuangalia ambacho wanahitaji baada ya Kocha Jackson Mayanja kukabidhi ripoti.
“Sisi tunaangalia ripoti ya mwalimu na nini kinahitajika, kawaida tunafanya mambo kwa nidhamu kubwa,” alisema.
Simba wameamua kufanya mambo yao kimya kwa kuwa wamelalamika wachezaji wengi wa kigeni waliwaangusha mwishoni baada ya wengine kufanya makusudi kuwakwamisha mwishoni.
Hivyo kwa sasa usajili kwao limekuwa ni jambo la umakini mkubwa ili kuepuka kufeli tena.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: