Posted by On the spot Tz
2:56:00 AM
0
Kwa mara nyingine serikali ya Kenya imepiga marufuku maandamano ya aina yoyote ya wafuasi wa muungano wa CORD unaoongozwa na waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo Raila Odinga, ili kushinikiza viongozi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kung'atuka madarakani.
Siku mbili ikiwa zimepita tokea kujiri maandamano ya wapinzani katika mji wa Kisumu yaliyosababisha mtu mmoja kuuawa na wengine sita kujeruhiwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya imepiga marufuku maandamano kama hayo nchini humo. Kwa mujibu wa wizara hiyo maandamano na machafuko yanayofanywa na wapinzani nchini humo yanakinzana na mapendekezo ya mahakama ya katiba ambayo ilikuwa imependekeza kudhaminiwa sheria za waandamanaji kwa upande mmoja, na kudhaminiwa usalama wa polisi kutoka kwa waandamanaji kwa upande wa pili. Kufuatia hali hiyo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya imeonya vikali juu ya mwendelezo wa matukio hayo ya upinzani. Kwa kipindi cha wiki sita sasa wapinzani nchini Kenya wamekuwa wakifanya maandamano yenye lengo la kushinikiza viongozi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kuondoka madarakani kwa kile kinachotajwa na wapinzani kuwa, tume hiyo haina tena itibari ya kusimamia uchaguzi mkuu wa mwakani nchini humo.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: