Posted by On the spot Tz
2:56:00 AM
0
Kwa mara nyingine serikali ya Kenya imepiga marufuku maandamano ya aina yoyote ya wafuasi wa muungano wa CORD unaoongozwa na waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo Raila Odinga, ili kushinikiza viongozi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kung'atuka madarakani.
Siku mbili ikiwa zimepita tokea kujiri maandamano ya wapinzani katika mji wa Kisumu yaliyosababisha mtu mmoja kuuawa na wengine sita kujeruhiwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya imepiga marufuku maandamano kama hayo nchini humo. Kwa mujibu wa wizara hiyo maandamano na machafuko yanayofanywa na wapinzani nchini humo yanakinzana na mapendekezo ya mahakama ya katiba ambayo ilikuwa imependekeza kudhaminiwa sheria za waandamanaji kwa upande mmoja, na kudhaminiwa usalama wa polisi kutoka kwa waandamanaji kwa upande wa pili. Kufuatia hali hiyo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya imeonya vikali juu ya mwendelezo wa matukio hayo ya upinzani. Kwa kipindi cha wiki sita sasa wapinzani nchini Kenya wamekuwa wakifanya maandamano yenye lengo la kushinikiza viongozi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC kuondoka madarakani kwa kile kinachotajwa na wapinzani kuwa, tume hiyo haina tena itibari ya kusimamia uchaguzi mkuu wa mwakani nchini humo.

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: