Posted by On the spot Tz
2:58:00 AM
0
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, ujamali uliomo katika maneno ya Qur'ani Tukufu ni muujiza na ni mlango wa kuvutiwa na mafundisho aali na yenye maana pana ya aya hizo.
Ayatullah Ali Khamenei alisema hayo jana jioni kwenye jalsa iliyojaa nuru ya Qur'ani Tukufu, katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani na kubainisha kwamba: Utulivu wa kiroho na kidini, ni moja ya baraka za kuyaelewa vizuri mafundisho ya Qur'ani na kwamba utulivu huo huandaa mazingira ya kuongezeka imani ya watu kwa Mwenyezi Mungu na kwa nguvu Zake. Ayatullah Khamenei amesema kuwa, leo hii dunia inahitajia mno mafundisho ya Qur'ani Tukufu kuliko wakati mwingine wowote na kusisitiza kwamba: Lau kama maana pana ya aya za Qur'ani Tukufu watabainishiwa watu kwa lugha nyepesi na ya kisasa, bila ya shaka yoyote athari zake zitakuwa kubwa sana, na zitaandaa uwanja wa kupatikana maendeleo ya kweli ya mwanadamu kwa sababu heshima, nguvu, ustawi wa kidunia, kuimarika kimaanawi, kupanuka fikra na itikadi na kuwa na furaha na utulivu moyoni, yote hayo yanategemea namna tutakavyotekeleza kivitendo mafundisho ya Qur'ani Tukufu. Aidha ameelezea kufurahishwa kwake na namna vijana wa Iran wanavyozidi kujiimarisha ki-Qur'ani na kusema kuwa, kama mafundisho ya Qur'ani yatazingatiwa inavyotakiwa, bila ya shaka yoyote dunia itaokoka kutoka katika vimbunga vya matatizo yake yote ambayo ni mengi sana leo hii.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: