Posted by On the spot Tz
6:24:00 PM
0
Baada
ya Yanga kuandika barua kwa Shirikisho la SokaTanzania (TFF), kuomba
ipate nafasi ya kumtumia Hassan Kessy, Simba wamelizungumzia suala hilo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema jeuri ndiyo
iliwaponza Yanga hadi suala kufikia lililopo sasa, hivyo wanatakiwa
kubadilika na kuwa waungwana na kuachana na majivuno.
Hans
Poppe 'raia' wa Iringa, amesema kama Yanga wanataka kumtumia Kessy,
waandike barua na iwe ya kiungwana, nao watajibiwa kiungwana.
"Sisi ni waungwana kweli, lakini kama mtu atakuwa anaonyesha dharau, anasema yeye ni timu ya wananchi basi tuone itakuwaje.
"Lakini
kama ni muungwana, basi anajibiwa kiungwana. Wao waandike barua na sisi
tutaona iko vipi. Kama wataandika na barua itaonekana si ya kiungwana,
basi wasubiri kumtumia baadaye baada ya pingamizi za usajili kupita,"
alisema Hans Poppe ambaye ni mwanajeshi mstaafu.
Yanga
ilishindwa kumtumia Kessy katika mechi yake dhidi ya Mo Bejaia nchini
Algeria baada ya blog hii kuandika kwamba kulikuwa na tatizo.
Msemaji wa TFF, Alfred Lucas amesema kweli Yanga wameishawasilisha barua hiyo na wanategemea uungwana wa Simba kulimaliza hilo.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: