Posted by On the spot Tz
2:38:00 AM
0
Siku moja baada ya mlinzi wa kati wa Mtibwa Sugar, Andrew Vicent ‘Dante’ kumwaga wino wa miaka miwili Jangwani, Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime ameibuka na kusema kuwa siyo huyo tu wakitaka wabomoe kikosi kizima na Mtibwa itabaki palepale.
Nahodha huyo wa zamani wa Taifa Stars amesema ni kutokana na timu kubwa za Yanga, Simba kuigeuza Mtibwa kama akademi yao, ameamua kuja na falsafa mpya ya usajili dakika za mwisho kabisa mwa dirisha baada ya kujua safu ipi imepungukiwa.
Maxime aliongeza kuwa kuondoka kwa Dante si ajabu wala pengo kikosini kwake kwani ana fursa za kutosha kupata mbadala wake, ikiwemo michuano ya Ndondo Cup inayoendelea katika viwanja mbalimbali jijini Dar kwani naye ‘aliokotwa’ hukohuko alipokuwa daraja la pili kwenye timu ya Kariakoo Lindi ya Mtwara.
“Wao wabomoe tu, wakitaka wachukue wote. Dante siyo pengo kwetu na mbadala wake atapatikana tu mwishoni mwa usajili. Kama yeye miaka miwili tu amefanikiwa kwenye timu kubwa, nini kinashindikana kupata mbadala wake?
“Mwenyewe nilimuokota daraja la pili, nikamtengeneza msimu mmoja tu, akaitwa timu ya taifa (chini ya kocha Mart Nooij), leo anasajiliwa Yanga, sina shaka naamini kina Dante ni wengi sana Tanzania hii, hata kwenye Ndondo Cup naweza kuwapata wengi tu,” anasema Maxime.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: