Posted by On the spot Tz
2:42:00 AM
0
Klabu ya Azam FC imetangaza kuwa, inasubiri makocha wake raia wa Hispania, Zeben Hernandez na Jonas Garcia warejee nchini ndiyo waanze kuangalia namna ya kuwakata baadhi ya wachezaji wanaoona hawatawafaa kwa msimu ujao.
Kumekuwa na taarifa kwamba, Azam inatarajia kuwapunguza wachezaji kumi kutoka kwenye kikosi chao wakiwemo wale waliomaliza mikataba yao lakini imekuwa ngumu kwa majina ya wachezaji hao kuwekwa hadharani.
Hata hivyo tayari Mkenya, Allan Wanga na Mrundi, Didier Kavumbagu, wapo kwenye orodha hiyo ya watakaoachwa.
Msimu ujao Azam itakuwa na kocha mkuu mpya ambaye ni Hernandez huku Garcia akiwa ni kocha wa viungo, hiyo ni baada ya timu hiyo kuachana na Stewart Hall raia wa Uingereza.
Akizungumzia ishu nzima ya usajili wa klabu hiyo, Mtendaji Mkuu wa Azam, Saad Kawemba amesema, Julai Mosi, mwaka huu, wachezaji wao wote wanatarajia kuingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya, na hapo ndipo makocha wao hao watakuwa wamesharejea na kuanza mchakato wa usajili ikiwemo kuwakata baadhi ya wachezaji.
“Kwa sasa hatuwezi kuanza mchakato wa usajili mpaka makocha wetu wale warejee, tunatarajia Julai Mosi watakuwa tayari nchini kwa kuanza kazi kwani siku hiyo pia ndiyo tunaanza kambi yetu ya kujiandaa na msimu mpya.
“Ishu za nani anaachwa na nani anaongezwa, wao ndiyo wataifanya kwani kabla ya kuondoka walipata fursa ya kukiona kikosi na kutambua wachezaji waliokuwa tayari kufanya nao kazi,” alisema Kawemba.
SOURCE: CHAMPIONI
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: