Posted by On the spot Tz
1:40:00 AM
0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amelimwa kadi ya njano timu yake KRC Genk ikifungwa mabao 3-1 na Club Brugge katika mchezo wa mchujo wa Ligi Kuu ya Ubelgiji kuwania kucheza michuano ya Ulaya.
Mchezo huo wa ugenini uliofanyika Uwanja wa Jan Breydelstadion mjini Brugge, Samatta alilimwa kadi hiyo dakika ya 76, ambayo inakuwa ya pili tangu ajiunge na timu hiyo Januari mwaka huu akitokea TP Mazembe ya DRC.
![]() |
Katika mchezo huo, kwa mara ya kwanza Samatta alicheza dakika zote 90 jahazi la timu yake likizama kwa mabao ya Waholanzi beki Stefano Denswil dakika ya 21, kiungo Ruud Vormer dakika ya 43 na kiungo Myahudi, Lior Refaelov dakika ya 60.
Bao pekee la Genk leo limefungwa na mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis dakika ya 89.
Samatta leo amecheza mechi ya 12 tangu ajiunge na Genk akitoka kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Afrika na TP Mazembe pamoja na kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora Anayecheza Afrika.
Katike mechi hizo, ambazo tano tu alianza, mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba SC ya Dar es Salaam, amefunga mabao nne, moja katika kila mechi Genk ikishindia 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji SV Zulte-Waregem, 4-0 na 4-1 dhidi ya KV Oostende na 3-2 dhidi ya Club Brugge mchezo wa kwanza.
Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: