Papa  Francis
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesisitizia umuhimu wa kutatuliwa mgogoro wa Syria kwa njia ya mazungumzo tu.
Sanjari na kuonyesha masikitiko yake makubwa kwa raia wa Syria ambao kutokana na njama za maadui wa taifa hilo, wanapitia hali ngumu kimaisha, amezitaka pande husika katika mgogoro huo kukaa pamoja kwa mazungumzo. Papa Francis amesema kuwa, mazungumzo ndiyo njia pekee ya kufikiwa amani na usalama nchini Syria. Kadhalika kiongozi huyo wa kanisa Katoliki amesisitiza juu ya ulazima wa pande husika kuheshimu usitishaji vita. Hii ni katika hali ambayo Wizara ya Ulinzi ya Russia pia imetangaza kuwa katika kuendeleza mpango wa 'Ukimya wa Serikali' pande za Moscow na Washington kwa upande mmoja na kadhalika Damascus na wapinzani kwa upande wa pili, wamekubaliana kusitisha mapigano kwa muda wa siku mbili nyingine katika viunga vya mji wa Damascus. Mpango huo wa usitishaji vita ulianza tangu tarehe 30 mwezi uliopita wa April kwa muda wa masaa 24 katika eneo la Ghouta ya mashariki, huko mashariki mwa mji wa Damascus na masaa 72 katika maeneo ya kaskazini ya Latakia.
«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post


No comments:

Leave a Reply