Posted by On the spot Tz
12:29:00 AM
0
Afrika Kusini na Zimbabwe zimewarejesha nyumbani raia 197 wa Msumbiji. Hayo yamesemwa na Idhaa ya Taifa ya Msumbuji.
Idara ya Taifa ya Uhamiaji nchini Msumbiji imeripoti kuwa, kufikia mwishoni mwa wiki iliyopita, raia 175 wa nchi hiyo walikuwa wameingia nchini kupitia mpaka wa Ressano Garcia wakitokea Afrika Kusini. Taarifa ya idara hiyo imeongeza kuwa, raia 22 wa nchi hiyo wamerejea nchini kufikia mwishoni mwa wiki jana kupitia vituo vya mpakani vya Machipanda na Ponta D'ouro katika mkoa wa Maputo, wakitokea Zimbabwe.
Itakumbukwa kuwa, raia 674 wa Msumbiji walirejeshwa nchini mwao na serikali ya Afrika Kusini mwaka jana 2015. Mamia ya raia wa Msumbuji wanaishi kama wakimbizi katika nchi mbali mbali zinazopakana nayo.
Kwa mujibu wa Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR, mwaka huu pekee, zaidi ya raia 10,000 wa Msumbiji wametorokea nchini Malawi kutokana na machafuko na uhasama kati ya serikali na chama kikuu cha upinzani cha Renamo, haswa katika mkoa wa Tete.
Septemba mwaka jana, Afrika Kusini ilisema kuwa takriban raia 2,600 wa Msumbiji wako katika magereza ya nchi hiyo huku 160 miongoni mwao wakitumikia vifungo vya maisha jela.
Afrika Kusini ni mwenyeji wa raia zaidi ya 40,000 wa Msumbiji, ambapo 32,000 miongoni mwao wanafanya kazi katika migodi na wengine 12,000 ni wakulima.

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: