Posted by On the spot Tz
4:10:00 AM
0
Beki Hassan Kessy amemvaa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na kumwambia asipotoshe umma na badala yake awaambie ukweli mashabiki na siyo kumtaja yeye ndiyo chanzo cha kukosa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.
Hiyo ni siku chache tangu Aveva ataje sababu ya timu hiyo kukosa ubingwa huo uliochukuliwa na Yanga.
Beki huyo, tayari amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuichezea Yanga kwa dau la shilingi milioni 40 huku akilipwa mshahara wa shilingi milioni 2 kwa mwezi.
Kessy alisema alichokifanya rais huyo ni kumtumia kama mwamvuli kuwafunika viongozi hao ili wasionekane kikwazo cha wao kushindwa kuiwezesha timu hiyo kutwaa taji hilo.
Kessy alisema kwanza kabisa aliondoka Simba ikiwa timu hiyo imebakiza michezo mingi ambayo kama viongozi na benchi la ufundi wangefanya kazi yake vizuri, ingechukua taji hilo, hivyo anashangaa yeye kutajwa.
Aliongeza kuwa, viongozi hao wasiitumie njia hiyo kumharibia kwa baadhi ya mashabiki wa timu hiyo huku akipanga kwenda kuwavaa mabosi hao akidai malipo yake ya mshahara wa mwezi uliopita baada ya kupata taarifa za malipo hayo.
“Kwanza hao viongozi wa Simba wasijisahaulishe kabisa, wakumbuke ninawadai malipo yangu ya mshahara wa mwezi uliopita, tayari nimeshamwambia katibu wao ninataka mshahara wangu, ni baada kutoona fedha kwenye akaunti yangu.
“Kwa sababu hao viongozi wanajifanya wajanja, bila aibu kabisa wanatangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mimi ndiyo sababu ya timu kushindwa kuchukua ubingwa wa ligi kuu, hivi ni kweli hicho walichokiongea!
“Kiukweli kabisa kwanza mashabiki ni mashahidi, mimi niliondoka Simba mapema, baada ya kuona ninatengwa na viongozi, walifungwa mechi na Mwadui FC, nilikuwepo na walipokwenda kucheza na Majimaji na kutoka suluhu nilikuwepo, viongozi hao hawana hoja, ni vema wakawaambia ukweli mashabiki,” alisema Kessy.
SOURCE: CHAMPION
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: