Posted by On the spot Tz
10:44:00 PM
0
Bayern Munich imeng’olewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya licha ya kushinda kwa mabao 2-1 ikiwa nyumbani Munich, Ujerumani.
Atletico Madrid imesonga kwenda fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa bao la ugenini baada ya ushindi wa bao 1-0 ikiwa nyumbani Madrid.
Kusonga mbele kwa Atletico Madrid, maana yake Kocha Pep Guardiola ambaye anaondoka kwenda kujiunga na Manchester City, ameshindwa kutimiza ndoto yake ya kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Bayern.
Mechi ilikuwa ngumu na tamu kuangalia na wenyeji walianza kupata bao katika dakika ya 31 kupitia Xabi Alonso.
Lakini Antoine Griezmann akaisawazishia Atletico kabla ya Robert Lewandowski kuongeza la pili.
Kila timu ilikosa penalti wakianza Bayern kupitia Thomas Muller na upande wa Atletico, Fernando Torres naye akakosa, makipa wa timu zote wakiwa mashujaa kwa kuzipangua.
Atletico Madrid inasubiri mshindi kati ya Real Madrid dhidi ya Manchester City katika mechi itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu jijini Madrid.
Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: