Rais Paul Kagame wa Rwanda ametoa mwito kwa bara la Afrika kutumia fursa zinazoletwa na mapinduzi ya nne ya viwanda ili kujifanya kuwa mdau kamili wa mambo ya dunia.
Rais Kagame ametoa mwito huo kwenye ufunguzi wa mkutano wa baraza la uchumi wa dunia kwa Afrika jana mjini Kigali. Amesema kama teknolojia na masoko ya mitaji yakitumiwa vizuri, yanaweza kulisaidia bara la Afrika kuondokana na changamoto zilizopo sasa.
Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Bw Akinwumi Adesina pia amesema Afrika haina chaguo ila kukumbatia mapinduzi ya nne ya viwanda, na moja ya vipaumbele katika hilo ni kuhakikisha watu wote wanapata umeme na wanaweza kutumia teknolojia za digitali.
Pamoja na kuwa soko la mitaji limetajwa kuwa na mustakbali mzuri, gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bw Benno Ndulu amesema tatizo lililopo ni kwamba benki kubwa zimejikita kwenye nchi chache tu.
«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post


No comments:

Leave a Reply