
Posted by On the spot Tz
2:44:00 PM
0

Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys wamepata sare nyingine baada ya Malaysia kusawazisha mabao yote mawili waliyotangulia kufunga vijana hao.
Mechi hiyo ni ya michuano ya Kombe la Vijana la AIFF inayofanyika katika mji wa Goa nchini India.
Boys walianza kupata bao lao la kwanza katika dakika ya 31 kupitia mshambuliaji wao hatari, Asad Ali Juma na Yohana Oscar akaongeza la pili katika dakika ya 59, ikiwa ni dakika chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.
Makosa ya walinzi, yaliwaruhusu Malaysia kusawazisha mabao yote mawili ndani ya dakika tano tu.
Walianza kupata bao la kwanza katika dakika ya 63 kupitia Arif Suhaimi na Najmi Idhar akafunga la pili katika dakika ya 68.
Hii ni sare ya tatu kwa Boys zikiwemo zile za 1-1 dhidi ya Marekani, 2-2 dhidi ya Korea na imepata ushindi mmoja wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji India. Inaendelea kuwa haijapoteza hata mechi moja katika michuano hiyo.

Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: