
Posted by On the spot Tz
7:01:00 AM
0
BUNGE la Uganda limeipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuwa na Baraza la
Maadili lenye nguvu kuliko nchi nyingine Afrika ambalo linashughulikia
watumishi wa umma ikiwemo kupambana na vitendo vya rushwa.
Akizungumza katika mkutano kati ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ya Uganda na Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma jana Dar es Salaam, Kiongozi wa kamati hiyo, Jacob Oboth-Oboth alisema kuwa katika nchi za Afrika, Tanzania pekee ndio lenye baraza imara na kwamba huenda Nigeria ndio inafuata.
Oboth ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Budama Kusini Wilaya ya Tororo, Uganda, alisema sababu ya kuja nchini ni kujifunza namna sekretarieti hiyo inavyofanya kazi kutokana na kupewa meno na sheria iliyopo kwenye Katiba.
"Uganda tuna mpango wa kufanya marekebisho ya sheria iliyotungwa mwaka 2002 kwa lengo la kuwa na watumishi wawajibikaji na utawala bora na kwamba bila ya kujifunza hawawezi kujua uzoefu uliopo na namna ya kuondokana na changamoto hizo," alisema.
Kamishna wa Maadili ya Utumishi wa Umma nchini, Jaji Salome Kaganda alisema wabunge hao wa Uganda waliomba kuja kubadilishana uzoefu na Sekretarieti ya Maadili ya Tanzania ili kuona inavyofanya kazi.
"Tumewashauri kwamba baraza letu ni chanzo cha Katiba ya mwaka 1977 na makatazo yake yamebainishwa katika katiba. Mfano, mbunge akionekana na hatia kinyume na katiba, anapoteza sifa kwamba haruhusiwi kugombea kwa miaka mitano kupigwa faini au kupewa onyo," alisema Jaji Kaganda.
Alifafanua kuwa walichokuja kujifunza wabunge wa Uganda ni kutokana na sheria yao ya maadili kuwepo kwenye vitabu vya sheria pekee wakati kinachotakiwa, sheria itakayotungwa iendane na katiba yenyewe ili kuipa meno.
onthespottz.blogspot.com
Akizungumza katika mkutano kati ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ya Uganda na Sekretarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma jana Dar es Salaam, Kiongozi wa kamati hiyo, Jacob Oboth-Oboth alisema kuwa katika nchi za Afrika, Tanzania pekee ndio lenye baraza imara na kwamba huenda Nigeria ndio inafuata.
Oboth ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Budama Kusini Wilaya ya Tororo, Uganda, alisema sababu ya kuja nchini ni kujifunza namna sekretarieti hiyo inavyofanya kazi kutokana na kupewa meno na sheria iliyopo kwenye Katiba.
"Uganda tuna mpango wa kufanya marekebisho ya sheria iliyotungwa mwaka 2002 kwa lengo la kuwa na watumishi wawajibikaji na utawala bora na kwamba bila ya kujifunza hawawezi kujua uzoefu uliopo na namna ya kuondokana na changamoto hizo," alisema.
Kamishna wa Maadili ya Utumishi wa Umma nchini, Jaji Salome Kaganda alisema wabunge hao wa Uganda waliomba kuja kubadilishana uzoefu na Sekretarieti ya Maadili ya Tanzania ili kuona inavyofanya kazi.
"Tumewashauri kwamba baraza letu ni chanzo cha Katiba ya mwaka 1977 na makatazo yake yamebainishwa katika katiba. Mfano, mbunge akionekana na hatia kinyume na katiba, anapoteza sifa kwamba haruhusiwi kugombea kwa miaka mitano kupigwa faini au kupewa onyo," alisema Jaji Kaganda.
Alifafanua kuwa walichokuja kujifunza wabunge wa Uganda ni kutokana na sheria yao ya maadili kuwepo kwenye vitabu vya sheria pekee wakati kinachotakiwa, sheria itakayotungwa iendane na katiba yenyewe ili kuipa meno.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
KIMATAIFA

On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.You May Also Like
Uhuru Kenyata Akanusha Kuwepo Mvutano Wa Kiuchumi Kati Ya Tanzania Na Kenya,,,,,,,,,,.,,,,
Mujuru kuungana na MDC ili kumuondoa Mugabe,,,,,,,,
Waziri Mkuu, David Cameron atangaza kujiuzulu baada ya Uingereza kupiga kura ya kujitoa rasmi kwenye Umoja wa Ulaya(EU).,,,,,,,,,,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
- quantalfaggart says:
Best Casinos in Las Vegas, NV - Mapyro
The best casinos in Las... more
Pageviews
65,292
No comments: