Posted by On the spot Tz
12:39:00 AM
0
Kikosi cha Simba kilichokwenda mkoani Dodoma kujiweka sawa kwa ajili ya michezo ijayo ya Ligi Kuu Bara, kimerejea jijini Dar es Salaam jana Jumapili na kutamba kuwa ipo ‘full tank’ kwa ajili ya kutoa dozi katika mechi zilizo mbele yao.

Simba ilikwenda mkoani humo baada ya kupata mwaliko wa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Dodoma inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Hata hivyo, kocha msaidizi wa timu hiyo, Mganda, Jackson Mayanja, amesema kwamba kupata safari hiyo pamoja na kucheza mchezo huo wakati ligi kuu imesimama, imekuwa ni faida kubwa kwao katika kujiweka sawa na kurekebisha waliyoyaona katika mechi zao mbili za awali, hivyo sasa wamekuwa fiti zaidi katika kila sekta.
“Mazoezi na mechi tuliyocheza Dodoma imekuwa na mchango mkubwa kwa maandalizi na kujiweka fiti zaidi kwa ajili ya michezo inayokuja, imekuwa vyema kupata nafasi ya kuja sehemu kama hii wakati ligi imesimama na kupata muda wa kurekebisha tuliyoyaona kwenye mechi za awali za ligi.
“Bado safari ni ndefu na ligi ina mechi nyingi, kwa hiyo unapopata nafasi kama hii na unapoitumia vizuri, inaleta faida kubwa kwa mechi za baadaye, ukizingatia msimu huu tunahitaji kufanya vizuri zaidi,” alisema Mayanja.
Mpaka sasa, Simba imecheza mechi mbili za ligi, ya kwanza waliumana na Ndanda na kushinda kwa mabao 3-0, mechi ya pili wakatoka suluhu dhidi ya JKT Ruvu, jumla imekusanya pointi nne. Keshokutwa Jumatano wanatarajia kucheza dhidi ya Ruvu Shooting.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: