Posted by On the spot Tz
12:45:00 AM
0
MBWANA ALLY SAMATA.
Straika Mbwana Samatta wa KRC Genk amesema Yanga kama ikijipanga inaweza kuifunga TP Mazembe katika mechi yao ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga itacheza na TP Mazembe ya DR Congo kati ya Juni 28 na 29, mwaka huu jijini Dar es Salaam mchezo wa kwanza wa Kundi A la Kombe la Shirikisho.
Samatta aliyewahi kuichezea TP Mazembe akitokea Simba, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, Yanga inaweza kuiondoa TP Mazembe katika michuano hiyo kama ikijipanga ipasavyo.
Alisema anaamini hilo linawezekana kwani kikosi cha Yanga hivi sasa kipo vizuri ukilinganisha na misimu mingine iliyopita.
“Hali hiyo ndiyo inayonifanya niamini kuwa Yanga inaweza kuifunga TP Mazembe, kwani nimekuwa nikiifuatilia sana na kuona jinsi wachezaji wake wanavyopambana uwanjani.
“Hata hivyo Yanga wanatakiwa kujipanga na kukiandaa kikosi chao kwa ajili ya michuano hiyo, kama kuna upungufu ambao waliuona hapo awali basi muda huu ndiyo wa kuufanyia kazi kabla ya kuanza kwa hatua hiyo makundi.
“TP Mazembe ni timu nzuri na yenye mafanikio Afrika, lakini katika soka lolote linaweza kutoka ndiyo maana nimesema Yanga inaweza kuifunga timu hiyo kama ikijiandaa vizuri,” alisema Samatta ambaye leo ataichezea Taifa Stars dhidi ya Misri.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: