Posted by On the spot Tz
12:40:00 AM
0
Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amesema anatamani kumtumia nahodha na beki wa kati wa zamani wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lakini hawezi kumlazimisha baada ya kukataa.
Cannavaro hivi karibuni alitangaza kustaafu kuichezea Taifa Stars ikiwa ni siku chache tangu anyang’anywe cheo cha unahodha na kupewa mshambuliaji wa KRC Genk ya Ubelgji, Mbwana Samatta.
Beki huyo baada ya kunyang’anywa cheo hicho haraka alitangaza kustaafu kuichezea Taifa Stars na kubaki na klabu yake ya Yanga iliyotinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika.
CANNAVARO |
Mkwasa alisema yeye alikuwa akihitaji uzoefu mkubwa alionao Cannavaro wa kucheza mechi nyingi za ya kimataifa, hivyo anaamini angekuwepo kikosi chake kingeimarika.
“Nilikuwa nahitaji uzoefu wa Cannavaro katika timu, lakini kutokana na yeye mwenyewe kuamua kukataa kujiunga nasi, nimeona nimuache nisiendelee kumlazimisha.
“Mimi sina taarifa za yeye kustaafu na hata hiyo barua aliyosema ameandika haijanifikia, hivyo nimeamua kumuacha, wapo vijana wengine nitakaowatumia,” alisema Mkwasa.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, akizungumzia hali hiyo, alisema: “Hatujapokea barua ya Cannavaro kustaafu kuichezea Taifa Stars, ndiyo maana aliitwa.”
Lakini Cannavaro alipotafutwa alisema: “Barua nimewapelekea siku nyingi tu na nasisitiza kuwa nimestaafu kuichezea Taifa Stars.”
Mkwasa alimuita Cannavaro ili aichezee Taifa Stars mechi ya leo dhidi ya Misri ya Kundi G kuwania kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon), lakini beki huyo amegoma.
SOURCE: CHAMPIONI

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: