Posted by On the spot Tz
12:40:00 AM
0
Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amesema anatamani kumtumia nahodha na beki wa kati wa zamani wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lakini hawezi kumlazimisha baada ya kukataa.
Cannavaro hivi karibuni alitangaza kustaafu kuichezea Taifa Stars ikiwa ni siku chache tangu anyang’anywe cheo cha unahodha na kupewa mshambuliaji wa KRC Genk ya Ubelgji, Mbwana Samatta.
Beki huyo baada ya kunyang’anywa cheo hicho haraka alitangaza kustaafu kuichezea Taifa Stars na kubaki na klabu yake ya Yanga iliyotinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika.
| CANNAVARO |
Mkwasa alisema yeye alikuwa akihitaji uzoefu mkubwa alionao Cannavaro wa kucheza mechi nyingi za ya kimataifa, hivyo anaamini angekuwepo kikosi chake kingeimarika.
“Nilikuwa nahitaji uzoefu wa Cannavaro katika timu, lakini kutokana na yeye mwenyewe kuamua kukataa kujiunga nasi, nimeona nimuache nisiendelee kumlazimisha.
“Mimi sina taarifa za yeye kustaafu na hata hiyo barua aliyosema ameandika haijanifikia, hivyo nimeamua kumuacha, wapo vijana wengine nitakaowatumia,” alisema Mkwasa.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, akizungumzia hali hiyo, alisema: “Hatujapokea barua ya Cannavaro kustaafu kuichezea Taifa Stars, ndiyo maana aliitwa.”
Lakini Cannavaro alipotafutwa alisema: “Barua nimewapelekea siku nyingi tu na nasisitiza kuwa nimestaafu kuichezea Taifa Stars.”
Mkwasa alimuita Cannavaro ili aichezee Taifa Stars mechi ya leo dhidi ya Misri ya Kundi G kuwania kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon), lakini beki huyo amegoma.
SOURCE: CHAMPIONI
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...



No comments: