Posted by On the spot Tz
2:54:00 PM
0
Kikosi
cha Yanga kimetua nchini tayari kuwavaa wapinzani wao TP Mazembe na
Kocha Hans van der Pluijm amesema vijana wake wako tayari.
Yanga imewasili kwa mafungu baada ya kundi la kwanza kutangulia na hilo la pili kutua usiku wa kuamkia leo.
“Kwa mazoezi tuliyofanya, marekebisho ya makosa ambayo tuliyaona baada ya mechi huko Algeria, tunaamini tuko tayari.
“Tunajua
TP Mazembe ni timu kubwa, lakini tunataka kupambana na kufanya vema,”
alisema Pluijm ambaye kikosi chake kiliwasili kwa mafungu.
Yanga
inatarajia kushuka dimbani keshokutwa Jumanne kuwavaa Mazembe katika
mechi ya Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments: