Posted by On the spot Tz
6:35:00 PM
0
Yanga
itakuwa dimbani Jumanne ijayo kuwavaa TP Mazembe katika mechi ya Kundi A
ya Kombe la Shirikisho Afrika linaloandaliwa na Shirikisho la Soka
Afrika (Caf) dhidi ya TP Mazembe, hofu kubwa ya timu hiyo ni beki ya
kushoto.
Wachezaji
wawili wanaocheza nafasi hiyo, Haji Mwinyi na Oscar Joshua wote wapo
katika hatari ya kuikosa mechi hiyo, hivyo Yanga ipo katika wakati mgumu
wa nani acheze nafasi hiyo.
Mwinyi
yeye ana kadi nyekundu aliyoonyeshwa katika mchezo uliopita wa michuano
hiyo dhidi ya MO Bejaia ya Algeria wakati Joshua ana maumivu ya nyama
za paja, pia aliyapata katika mchezo huo.
Habari
njema kwa Yanga ni kwamba, Joshua tayari ameanza mazoezi mepesi kambini
huko mjini Antalya, Uturuki ambako timu hiyo imejichimbia kujiandaa na
mechi dhidi ya TP Mazembe.
Kutoka
Uturuki, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh alisema: “Joshua anaendelea
vizuri na tayari ameanza mazoezi mepesi kwa ajili ya kujiandaa na mechi
na Mazembe.
“Bado
sijajua hatma yake kama atacheza au hatocheza mechi na Mazembe, hivyo
kila kitu kitajulikana ikiwa imebaki siku moja kabla ya mchezo wao baada
ya daktari wetu Edward Bavo kutoa ripoti yake.”
Joshua
alipata majeraha hayo usiku wa Jumapili iliyopita dakika ya 32 katika
mchezo dhidi ya MO Bejaia mjini Bejaia, Algeria ambapo ilibidi atolewe
na nafasi yake kuchukuliwa na Mwinyi. Katika mchezo huo, Yanga ilifungwa
bao 1-0.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: