Posted by On the spot Tz
2:57:00 PM
0
Mwenyekiti wa TLP taifa Dkt. Augustine Lyatonga Mrema amesema kwamba
kitendo cha Rais Dkt. John Magufuli kusema kwamba siasa ziachwe hadi
miaka mitano iishe kunatokana na tabia ya upinzani kugomea kila kitu
bila kuweka maslahi ya taifa mbele.
Dkt. Mrema ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumzia kuhusu kauli hiyo ya Rais na kama haitaviathiri vyama kikiwemo chama anachokiongoza cha TLP.
''Kwa maoni yangu binafsi hii imetokana na tabia yetu sisi wapinzani kugomea kila kitu hata mambo ambayo yana maslahi kwa taifa, kwa mfano ukiangalia wakati Rais Dkt. John Magufuli anazindua bunge la bajeti wapinzani walimgomea na kutoka nje, hapa walianza kumhukumu kabla hajaanza kazi''- Amesema Mrema.
Mrema ameongeza kuwa hata bunge la bajeti linaloendelea wabunge wa upinzani wametoka vikao karibu vyote wakati bajeti inayojadiliwa siyo ya Naibu Spika ni bajeti ya serikali na kwamba wangetumia kanuni za bunge kuweza kumuondoa kama hawamtaki kuliko kuacha kuwakilisha wananchi wao.
Aidha Mrema ameenda mbali na kusema kuwa nchi hii haiwezekani kila siku ikawa ni maandamano kwani wananchi wanatakiwa wafanye kazi na kama wapinzani walikuwa na nia ya dhati wangebakia bungeni wajadili kwanza bajeti.
Kuhusu chama chake pia kutofanya siasa Mrema amesema yeye hana maandamano ya kila mara hivyo anaamini atakuwa na mikutano halali muda ukifika lakini kwa sasa wananchi wafanye kazi kwanza.
onthespottz.blogspot.com
Dkt. Mrema ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumzia kuhusu kauli hiyo ya Rais na kama haitaviathiri vyama kikiwemo chama anachokiongoza cha TLP.
''Kwa maoni yangu binafsi hii imetokana na tabia yetu sisi wapinzani kugomea kila kitu hata mambo ambayo yana maslahi kwa taifa, kwa mfano ukiangalia wakati Rais Dkt. John Magufuli anazindua bunge la bajeti wapinzani walimgomea na kutoka nje, hapa walianza kumhukumu kabla hajaanza kazi''- Amesema Mrema.
Mrema ameongeza kuwa hata bunge la bajeti linaloendelea wabunge wa upinzani wametoka vikao karibu vyote wakati bajeti inayojadiliwa siyo ya Naibu Spika ni bajeti ya serikali na kwamba wangetumia kanuni za bunge kuweza kumuondoa kama hawamtaki kuliko kuacha kuwakilisha wananchi wao.
Aidha Mrema ameenda mbali na kusema kuwa nchi hii haiwezekani kila siku ikawa ni maandamano kwani wananchi wanatakiwa wafanye kazi na kama wapinzani walikuwa na nia ya dhati wangebakia bungeni wajadili kwanza bajeti.
Kuhusu chama chake pia kutofanya siasa Mrema amesema yeye hana maandamano ya kila mara hivyo anaamini atakuwa na mikutano halali muda ukifika lakini kwa sasa wananchi wafanye kazi kwanza.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: