Posted by On the spot Tz
4:33:00 AM
0
Kila siku asubuhi huwa nazisogeza
headlines zilizobebwa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania, Uchambuzi
wa stori zote napandisha kwenye account yangu ya facebook Tommachupa. Tayari nimezikusanya na waweza kuzipitia hapa
chini moja baada ya nyingine.
Stori kubwa kwenye magazeti ya leo June
09 2016 ni kuhusu Bajeti ya mwaka 2016/2017, moja ya stori iliyochomoza
ni hii kwenye gazeti la Nipashe yenye kichwa cha habari ‘Mikoa mitano maskini zaidi Tanzania hii hapa”
Serikali imesema kuwa Kigoma, Geita, Kagera, Singida na Mwanza ndiyo mikoa mitano maskini zaidi nchini, aidha mikoa ya Dar es salaam, Kilimajaro, Arusha, Pwani na Manyara ndiyo mikoa mitano yenye ahueni ya umaskini nchini
Waziri wa fedha na mipango Dk Phillip
Mpango alisema hayo jana wakati akiwasilisha bungeni taarifa ya hali ya
uchumi ya mwaka 2015 na mpango wa maendeleo wa taifa kwa mwaka wa fedha
2016/17.
Waziri Mpango alisema tathmini ya hali
ya umaskini kimaeneo iliyofanyika kwa kutumia takwimu za sensa ya watu
ya mwaka 2012 na utafiti wa hali ya kipato na matumizi katika kaya wa
mwaka 2012,unaonyesha matokeo chanya na kutofautiana kimkoa na wilaya
Waziri Mpango alisema mkoa wa Kigoma unaongoza kwa kuwa na umaskini mkubwa wa 48.9% ukifuatiwa na Geita (43.7%), Kagera (39.3%), Singida (38.2%) na Mwanza (35.3%).
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: