Posted by On the spot Tz
8:40:00 AM
0
JOSEPH OMOG.
Kocha Joseph Omog raia wa Cameroon ameingia kwenye rada za klabu ya Simba baada ya kumuweka katika listi ya makocha inaowataka.
Simba imeamua kuachana kabisa na suala la Wazungu na Omog aliyewahi kuinoa Azam FC na kuipa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara kwanza na ya mwisho atakuwa sehemu kati ya wanaotakiwa.
Hata hivyo, inaonekana chaguo la kwanza la Simba ni Kocha Kalisto Pasuwa anayekinoa kikosi cha timu ya taifa ya Zimbabwe.
Tayari onthespottz lilishaandika kuhusiana na Pasuwa ingawa Simba pia inamfuatilia kocha mwingine kutoka nchini Senegal.
“Kweli zoezi limekuwa likifanyika kwa ungalifu mkubwa. Tunahitaji muda na Simba inataka kufanya mambo kwa uhakika. Omog ni sehemu ya ambao wanaweza kupewa nafasi lakini si chaguo la kwanza,” kilieleza chanzo.
Simba imekuwa ikinolewa na Mganda Jackson Mayanja ambaye ni kocha msaidizi.
Hata hivyo, amekuwa ni kaimu kocha mkuu kwa kuwa Simba ilimtimua aliyekuwa Kocha Mkuu, Dylan Kerr raia wa Uingereza siku moja tu baada ya kumwajiri Mayanja ili amsaidie.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: