Posted by On the spot Tz
2:08:00 PM
0
Rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye alishinda katika uchaguzi wa mwezi Februari mwaka huu, Jana Alhamisi ameapishwa kuwa rais wa nchi hiyo kwa kipindi cha tano mfululizo.
Sherehe za kuapishwa Yoweri Museveni ambazo zimefanyika jijini Kampala, zimehudhuriwa na marais wa nchi kadhaa za Afrika akiwemo Rais Omar al Bashir wa Sudan.
Museveni (71) aliingia madarakani mwaka 1986 nchini Uganda na katika uchaguzi wa tarehe 18 Februari mwaka huu, ameshinda kwa asilimia 60.62 ya kura.
Waangaliaji wa kimataifa wamesema kuwa uchaguzi wa Rais nchini Uganda ulifanyika katika anga ya vitisho na hofu iliyosababishwa na miamala mibaya ya serikali.
Daktari Kizza Besigye, mmoja wa wagombea wa upinzani amekataa matokeo hayo na kujitangaza mshindi.
Jana polisi wa Uganda walimtia mbaroni Dakta Besigye. Baada ya kukamatwa Besigye, chama chake cha FDC kilisambaza mikanda ya video katika mitandao ya kijamii, inayoonyesha kiongozi wao huyo akiapishwa kama rais wa Uganda na kusema kuwa kiapo cha leo cha Rais Museveni si halali.

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: