Posted by On the spot Tz
2:04:00 PM
0
Baada ya Dk Ali Larijani, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) kufungua duru ya 33 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu jana Jumatano, mashindano hayo yameanza rasmi leo.
Mashindano hayo yameanza kwa kuchuanishwa washindanaji wa kuhifadhi Qur'ani nzima na qiraa na uhakiki wa Qur'ani.
Shirika la habari la IQNA limeripoti kuwa, mashindano ya qiraa na kuhifadhi Qur'ani nzima yamefanyika katika kumbi za hoteli walizofikia washindanaji hao mbele ya majaji wa kimataifa ikiwa ni hatua ya mchujo wa kuchagua watu wa kuingia kwenye ukumbi mkuu wa mashindano.
Itakumbukwa kuwa nchi 75 zina wawakilishi wao katika mashindano hayo. Hayo yamesemwa na Sheikh Ali Mohammadi Mwakilishi wa Faqihi Mtawala na Mkuu wa Taasisi ya Wakfu ya Iran ambaye ameongeza kwamba, kutakuwa na washiriki 130 kutoka nchi 75 katika mashindano hayo.
Amesema kwa mara ya kwanza mashindano hayo yanafanyika katika Ukumbi Mkubwa wa Swala wa Imam Khomeini MA hapa jijini Tehran, ili kuwezesha idadi kubwa ya watu kujumuika katika mashindano hayo.
Sheikh Ali Mohammadi ameongeza kuwa, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na washiriki kutoka mabara ya Afrika, Asia, Ulaya, Marekani na Pasifiki.
Mashindano hayo ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yanatarajiwa kumalizika siku ya Jumanne ya mwezi kumi Shaaban, sawa na tarehe 17 mwezi huu wa Mei.
Baada ya Dk Ali Larijani, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) kufungua duru ya 33 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu jana Jumatano, mashindano hayo yameanza rasmi leo.
Mashindano hayo yameanza kwa kuchuanishwa washindanaji wa kuhifadhi Qur'ani nzima na qiraa na uhakiki wa Qur'ani.
Shirika la habari la IQNA limeripoti kuwa, mashindano ya qiraa na kuhifadhi Qur'ani nzima yamefanyika katika kumbi za hoteli walizofikia washindanaji hao mbele ya majaji wa kimataifa ikiwa ni hatua ya mchujo wa kuchagua watu wa kuingia kwenye ukumbi mkuu wa mashindano.
Itakumbukwa kuwa nchi 75 zina wawakilishi wao katika mashindano hayo. Hayo yamesemwa na Sheikh Ali Mohammadi Mwakilishi wa Faqihi Mtawala na Mkuu wa Taasisi ya Wakfu ya Iran ambaye ameongeza kwamba, kutakuwa na washiriki 130 kutoka nchi 75 katika mashindano hayo.
Amesema kwa mara ya kwanza mashindano hayo yanafanyika katika Ukumbi Mkubwa wa Swala wa Imam Khomeini MA hapa jijini Tehran, ili kuwezesha idadi kubwa ya watu kujumuika katika mashindano hayo.
Sheikh Ali Mohammadi ameongeza kuwa, mashindano ya mwaka huu yatakuwa na washiriki kutoka mabara ya Afrika, Asia, Ulaya, Marekani na Pasifiki.
Mashindano hayo ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yanatarajiwa kumalizika siku ya Jumanne ya mwezi kumi Shaaban, sawa na tarehe 17 mwezi huu wa Mei.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: