Posted by On the spot Tz
1:15:00 AM
0

KIKOSI CHA YANGA KILICHOPO ANGOLA;
Makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’ na Deo Munishi ‘Dida’.
Mabeki; Juma Abdul, Mwinyi Haji, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Pato Ngonyani na Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro'.
Viungo; Thabani Kamusoko, Salum Telela, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Godfrey Mwashiuya.
Washambuliaji; Donald Ngoma, Matheo Anthony, Amissi Tambwe na Paul Nonga.
BENCHI LA UFUNDI;
Kocha Mkuu; Hans van der Pluijm (Uholanzi)
Kocha Msaidizi; Juma Mwambusi
Kocha wa makipa; Juma Pondamali
Daktari; Edward Bavu
Mchua Misuli; Jacob Onyango
Mtunza Vifaa; Mohammed Mpogolo
Meneja; Hafidh Saleh
WACHEZAJI WALIOBAKI DAR;
Benedicto Tinocco, Said Juma, Issoufou Boubacar na Malimi Busungu.

YANGA SC imewasili salama mjini Dundo, Angola baada ya safari ya kutwa nzima, tayari kwa mchezo wao wa kesho dhidi ya wenyeji, Sagrada Esperanca kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Baada ya kutua Luanda, Yanga iliunganisha ndege nyingine kwa saa mbili kwenda mji wa Dundo ambaako ni maskani ya Sagrada Esperanca.
Yanga imefikia katika hoteli ya bora zaidi mjini humo, Diamante naa leo Saa 9:00 Alasiri kikosi chake kitashuka kwenye Uwanja wa Sagrada Esperanca mjini hapa kufanya mazoezi.
Katika mchezo wa kesho, Yanga itahitaji sare ili kuingia hatua ya makundi, baada ya awali kushinda 2-0, mabao ya Simon Msuva na Matheo Anthony wiki iliyopita Dar es Salaam.
Kocha Mholanzi wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema kwamba ana imani kurejea kwa wachezaji wake wawili Wazimbabwe, kiungo Thabani Kamusoko na mshambuliaji Donaldo Ngoma kutaiogezea nguvu timu yake.
Mechi ya kesho itachezeshwa na marefa wa Madagascar, Hamada el Moussa Nampiandraza atakayepuliza filimbi, akisaidiwa na washika vibendera Velomanana Ferdinand Jinoro na Jean Thierry Djaonirina.
Yanga imeangukia katika kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Shirikisho, baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, ikilazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam na kufungwa 2-1 Alexandria.
![]() |
| Mwonekano wa Hoteli Diamante ambayo wamefikia Yanga SC kwa nje |
![]() |
| Hotel Diamanye ambayo wamefikia Yanga ina bwawa dogo la kuogelea |
| Hotel Diamante ambayo wamefikia Yanga SC ina gym nzuri ya mazoezi |
Yanga ilianza vizuri tu kwa kuzitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa jumla ya mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani kabla ya kuitoa na APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-1 Kigali na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Kwa upande wao, Sagrada Esperanca katika Raundi ya Awali waliitoa Ajax Cape Town ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 ugenini na kushinda 2-0 nyumbani. Katika Raundi ya kwanza wakaitoa LD Maputo ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 2-1 ikishinda 1-0 nyumbani na kutoa sare ya 1-1 ugenini na kwenda hatua ya 16 Bora, ambako waliitoa V. Club Mokanda ya Kongo kwa jumla ya mabao 4-1 wakishinda 2-1 ugenini na 2-0 nyumbani.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...




No comments: