Posted by On the spot Tz
8:03:00 AM
0
KLABU ya Yanga imepanga kufanya mabadiliko ya kulitumia basi lao ambalo walipewa na wadhamini wao Kampuni ya Bia (TBL) ambapo litakuwa maalum kwa mashabiki wao badala ya kutumiwa na wachezaji wao.
Hayo yamesemwa na Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro alipokuwa kwenye uzinduzi wa Tawi la Yanga Uswazi Mbeya eneo la Sokomatola juzi Jumatano wakati Yanga ilipokuwa jijini hapa kucheza na Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara.
Muro amesema uamuzi huo wameufikiria kwa kuwa wamekuwa wakitumia zaidi usafiri wa ndege ambao umezaa jina la wao kuitwa wa kimataifa pamoja na kushiriki michuano ya nje.
“Sisi ni watu wa angani tu muda wote, hivyo hata basi letu tumepanga kuwapa mashabiki walitumie kwa ajili ya kusafiri kuifuata timu kuipa sapoti, wale ndugu zetu wao ndiyo wa kutumia basi.
“Kwa mfano sisi tumeingia hapa asubuhi, tumetoka Dar saa 12 asubuhi, saa moja tumetua hapa, ila watani waliondoka Dar, jana asubuhi hadi leo (juzi) hawajafika Songea,” alisema Muro huku akishangiliwa na mashabiki wa Yanga waliokuwa eneo hilo.
“Msimu ujao pia tutashiriki katika michuano ya kimataifa, hivyo muda mwingi tutakuwa na safari za nje kama ilivyo msimu huu, hivyo hili basi letu litakuwa linatumika kuwafuata mashabiki na kuwapeleka mkoa mwingine pindi sisi tutakapokuwa tunasafiri kwa ndege,” aliongeza Muro.
Alisema kuwa ikiwa uamuzi huo utapitishwa, basi wao watakuwa wanasafiri kwa ndege tu hata katika safari za ndani na basi lao litakuwa linatumiwa na wachezaji katika safari za ndani ya Dar tu.
onthespottz.blogspot.com
Hayo yamesemwa na Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro alipokuwa kwenye uzinduzi wa Tawi la Yanga Uswazi Mbeya eneo la Sokomatola juzi Jumatano wakati Yanga ilipokuwa jijini hapa kucheza na Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu Bara.
Muro amesema uamuzi huo wameufikiria kwa kuwa wamekuwa wakitumia zaidi usafiri wa ndege ambao umezaa jina la wao kuitwa wa kimataifa pamoja na kushiriki michuano ya nje.
“Sisi ni watu wa angani tu muda wote, hivyo hata basi letu tumepanga kuwapa mashabiki walitumie kwa ajili ya kusafiri kuifuata timu kuipa sapoti, wale ndugu zetu wao ndiyo wa kutumia basi.
“Kwa mfano sisi tumeingia hapa asubuhi, tumetoka Dar saa 12 asubuhi, saa moja tumetua hapa, ila watani waliondoka Dar, jana asubuhi hadi leo (juzi) hawajafika Songea,” alisema Muro huku akishangiliwa na mashabiki wa Yanga waliokuwa eneo hilo.
“Msimu ujao pia tutashiriki katika michuano ya kimataifa, hivyo muda mwingi tutakuwa na safari za nje kama ilivyo msimu huu, hivyo hili basi letu litakuwa linatumika kuwafuata mashabiki na kuwapeleka mkoa mwingine pindi sisi tutakapokuwa tunasafiri kwa ndege,” aliongeza Muro.
Alisema kuwa ikiwa uamuzi huo utapitishwa, basi wao watakuwa wanasafiri kwa ndege tu hata katika safari za ndani na basi lao litakuwa linatumiwa na wachezaji katika safari za ndani ya Dar tu.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: