Posted by On the spot Tz
2:11:00 PM
0
Kundi moja nchini India limefanya maombi kumuombea ushindi mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump.
Kundi hilo kwa jina Hindu Sena, linaloegemea siasa za mrengo wa kulia, linasema linamuunga mkono Trump kwa sababu “ndiye tumaini pekee kwa binadamu katika vita dhidi ya ugaidi wa Kiislamu”.
Wafuasi kadha wa kundi la Hindu Sena waliwasha moto na kufanya maombi katika bustani moja mjini Delhi siku ya Jumatano.
Kadhalika walikuwa na bango la kutangaza uungwaji mkono wao kwa Bw Trump.
Walikuwa wamezungukwa na sanamu za miungu wa Kihindi.
"Ni Donald Trump pekee anayeweza kuokoa binadamu," Vishnu Gupta, mwanzilishi wa kundi hilo aliambia shirika la habari la Associated Press.
Aliambia gazeti la The Indian Express kwamba kundi hilo limepanga hafla kadha za kudhihirisha uungaji mkono wao wa dhati kwa Bw Trump.
Bw Trump amependekeza Waislamu wazuiwe kuindia Marekani, hatua iliyomfanya kushutumiwa vikali.
Wiki hii, baada ya meya wa London Sadiq Khan ambaye ni Mwislamu kusema huenda asipate fursa ya kuzuru Marekani iwapo Trump atashinda, mfanyabiashara huyo kutoka New York alijiteta kwamba baadhi ya mambo ni ya kipekee na meya huyo hawezi kuzuiwa.
Baadaye Bw Trump alionekana kulegeza msimamo zaidi na kusema hilo lilikuwa pendekezo tu.
Bw Trump pia ametetea kuuawa kwa familia za magaidi na kuvamiwa kwa Syria ili kuangamiza kundi linalojiita Islamic State na kutwaa mafuta.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: