Posted by On the spot Tz
1:14:00 PM
0
Siku moja baada ya Yanga kufanikiwa kunyakua ubingwa Kombe la FA, straika Mrundi, Amissi Tambwe, amesema yupo tayari kurudi Simba kama uongozi wa timu hiyo utamhitaji.
Hata hivyo, Tambwe ambaye ndiye mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu na ambaye pia juzi Jumatano aliiongoza Yanga kuifunga Azam FC mabao 3-1, katika mchezo wa fainali wa Kombe la FA alisema kuwa atafanya hivyo mara tu uongozi wa Simba utakapomuomba radhi kwa mabaya yote uliyomfanyia wakati akiitumikia klabu hiyo.
Tambwe alisema licha ya kuwa na furaha Yanga lakini anaionea huruma Simba ambavyo inataabika kuhakikisha inarudisha makali yake.
Alisema kitendo hicho kimekuwa kikimsononesha kwani hakutarajia kama ingekumbwa na hali hiyo kutokana na jinsi viongozi wa timu hiyo walivyokuwa wakijisifu baada ya kumfungashia virago kwa mbwembwe.
“Pamoja na yote hayo mimi huwa sina kinyongo kwani walifanya hivyo bila kujua nini kitatokea mbele yao na sasa najua watakuwa wanajuta kwa uamuzi wao huo wa kunifukuza klabu kwao.
“Hata hivyo, naomba kuwaambia kuwa kama wananihitaji na wanataka nirudi klabuni hapo basi waniombe radhi kwani walinidhalilisha sana, wakifanya hivyo mimi nipo tayari kurudi lakini nitakapomaliza majukumu yangu na klabu yangu ya Yanga ambayo inanithamini na ninaishi kwa amani,” alisema Tambwe.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: