Posted by On the spot Tz
8:52:00 AM
0
HAMIS KIIZA
Uongozi wa klabu ya Simba umetupa macho zaidi kwa wachezaji kutoka Afrika Magharibi na kuamua kuachana kabisa na wale wanaotokea Kenya na Uganda.
Taarifa za ndani kutoka Simba, zimeeleza wameamua kufanya hivyo baada ya kukerwa na mambo mengi yaliyotokana na Waganda na Wakenya.
Msimu uliopita, Simba ilisajili Waganda watano, lakini Emmanuel Okwi na Juuko Murshid pekee ndiyo walifanya vizuri huku wawili wakigeuka mizigo.
Msimu huu, Juuko alianza vizuri, mwishoni akadorora. Hamisi Kiiza akafunga mabao 19, lakini mwisho uongozi wa Simba ukamshutumu kuwa ni tatizo kubwa miongozi mwao.
"Kweli tumeamua tuangalie wachezaji Afrika Magharibi, maana Wakenya na Waganda wamegeuka tatizo kubwa na hawakuwa na 'pafomensi' nzuri kwa kweli. Waliofanya vizuri ni Kipa Angban na Majabvi ambao wanatokea Ivory Coast na Zimbabwe.
"Mkenya Paul Kiongera alikuwa majeruhi na alipopewa nafasi hakuonyesha chochote. Juuko umeona alichotufanyia mwishoni, hakuwa msaada hata kidogo.
"Achana na hivyo, rejea kwa Kiiza. Kafunga mabao mengi kweli, alikuwa msaada awali. Lakini mwisho ndiye kawa tatizo, utaona hata kufunga hakuwa akifunga lakini sisi tunajua kila kitu na siku moja tutaweka mambo hadharani kabisa," alisema kiongozi huyo.
"Sasa tunajaribu kutafuta wachezaji wa Afrika Magharibi ambao watakuwa wapya kabisa hapa Afrika Mashariki ili tuweze kujenga kikosi chenye uaminifu."
Kikosi cha Simba kimemaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu baada ya mabingwa Yanga, Azam FC wameshika nafasi ya pili.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: