Posted by On the spot Tz
1:57:00 AM
0
Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali, amemjia juu kipa wake, Deogratius Munishi ‘Dida’ baada ya kipa huyo mara kwa mara kufanya makosa ya kizembe ambayo huwapa wapinzani wao mabao ya mapema.
Pondamali ameweka wazi kuwa kwa siku za hivi karibuni, Dida amekuwa hana umakini anaposimama langoni na kufanya makosa ya kizembe, hivyo ameanza kumchunguza ili kubaini tatizo lake kwa kina.
Pondamali amesema kuwa makosa anayoyafanya Dida ni hatari sana kama watakutana na timu inayoweza kutumia makosa ya kipa, hivyo anafanya juu chini kutibu tatizo hilo kwani kama akimuacha anaweza kuwagharimu kwenye mechi zijazo na kuwafanya wakose ubingwa.
“Sielewi ana tatizo gani kwani kwenye mechi kama tatu mfululizo namuona hana umakini kabisa, mechi ya Coastal Union alifanya uzembe tukafungwa bao na kutupa shida ya kuchomoa na kuongeza, pia ile ya JKT Mgambo akafanya makosa yaleyale.
“Hii ni hatari kwetu kwa kipindi hiki tulichopo cha kusaka ubingwa, mpaka wakati mwingine namuuliza Dida unataka kuniua na presha maana simuelewi nini malengo yake ya anachokifanya, hivyo ni lazima nikae naye na kumchunguza nini kinamsibu mpaka kipindi hiki apoteze umakini golini, kikubwa kwa sasa tunataka ubingwa na si kingine,” alisema Pondamali.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: