Posted by On the spot Tz
2:12:00 AM
0
Hans Vand der Pluijm
Kazi safi iliyofanywa na benchi la ufundi la Yanga, imeonekana kuwakuna viongozi wa timu hiyo na kuvutiwa kuendelea na makocha hao akiwemo kocha wa makipa, Juma Pondamali aliyemaliza mkataba wake klabuni hapo hivi karibuni.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga, amesema benchi lao la ufundi limefanya vizuri na hata wakiliweka suala hilo mezani, watalifikiria pia katika uwiano wa juu katika kuendelea nao msimu ujao.
Ukiachana na Pondamali, pia Kocha Mkuu wa Yanga, Mdachi, Hans van Der Pluijm, naye anamaliza mkataba wake mwisho wa msimu huu.
“Nisingependa sana kulizungumzia hili, lakini ieleweke kuwa Yanga tuna taratibu zetu katika haya mambo lakini ukipimia uwiano, benchi la ufundi limefanya kazi nzuri sana, kwa hiyo kama kutakuwa na lolote la kufikiria basi litakuwa zaidi ya asilimia 50 tunaweza kuendelea nao,” alisema Sanga.
Ukiachana na Yanga kuchukua ubingwa mara ya pili mfululizo ikiwa chini ya Pluijm, lakini pia wiki iliyopita ilifanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho ikiwa ni mara ya kwanza kwa Yanga tangu ilipofanya hivyo mara ya mwisho mwaka 1998 kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: