Posted by On the spot Tz
3:48:00 AM
0
Mrisho Khalfan Ngassa
Pamoja na uongozi wa Free State Stars ya Afrika Kusini kumzuia kiungo wake mshambuliaji, Mrisho Ngassa kumtoa kwa mkopo, nyota huyo amewatoa hofu mashabiki wa Yanga na kuwaambia siku si nyingi anarejea kwenye klabu hiyo.
Ngassa ameitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuwasili nchini kisha kutazama mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa, Dar ambapo Yanga ilishinda mabao 3-1.
Ngassa alijiunga na Free State inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini, mwaka jana baada ya mkataba wake kumalizika Yanga.
Ngassa amesema viongozi wa Yanga ndio waliowafuata Free State kwa ajili ya kumuomba kwa mkopo ili aiongezee nguvu timu hiyo katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Ngassa alisema, bado mazungumzo yanaendelea kati ya pande hizo mbili kwa kushirikiana na yeye kuhakikisha anarejea Yanga.
“Nimefurahi sana kuonana na mashabiki wa Yanga na kunifurahia, wengi wao wameonekana kuwa na upendo na mimi waliponiona uwanjani, pia wakinihitaji nirejee kuiongezea nguvu timu hiyo kwenye michuano ya kimataifa.
“Hivyo niwatoe hofu tu kuwa mazungumzo yanaendelea vizuri kati ya Yanga na Free State timu inayonimiliki na Mungu akijalia, basi nitarejea kuichezea Yanga,” alisema Ngassa.
Alipotafutwa Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro alionekana kufichaficha mambo kwa kusema: “Hilo suala bado halijafika mezani kwangu, hivyo siwezi kulizungumzia. Ngassa bado ni mchezaji halali wa Free State, kwa hiyo mambo yakiwa tayari ndiyo naweza kulizungumzia.”
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: