Posted by On the spot Tz
5:54:00 AM
0

Ndege ya kivita ya Marekani aina ya B-52 imeanguka muda mfupi baada ya kupaa kutoka kwenye kambi ya taifa hilo eneo la Guam.
Jeshi la Marekani limesema wanajeshi wote saba waliokuwa kwenye ndege hiyo walifanikiwa kuruka salama kutoka kabla ya ndege hiyo kuteketea.
Ndege hiyo ilikuwa imepaa kutoka kituo cha jeshi cha Andersen.
Picha zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zimeonesha moshi mkubwa ukitanda angani kutoka kwa vifusi vya ndege hiyo.
Ndege hiyo, ambayo hutumiwa kuangusha mabomu, ilitumwa Guam kutoka jimbo la North Dakota na ni sehemu ya juhudi za Marekani za kuendeleza uwepo wake kijeshi katika bahari ya Pasifiki.
Gavana wa jimbo la Guam amenukuliwa na tovuti ya habari ya Kuam akisema kwamba halikuwa shambulio.
Ndege aina ya 5-52 zimetumiwa na Marekani kwa miaka 60 sasa, na zilichangia sana vita Vietnam na Afghanistan.
Guam ni jimbo linalomilikiwa na Marekani eneo la Micronesia, Pasifiki magharibi na hupatikana kilomita 6,000 magharibi mwa Hawaii.
Mwaka 2008, wanajeshi sita walifariki baada ya ndege aina ya B-52 kuanguka karibu na Guam.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: