Posted by On the spot Tz
7:15:00 AM
0
Straika wa Simba, Ibrahim Ajib aliyepo nchini Afrika Kusini ‘Sauz’ akifanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa, amesema anaendelea vizuri na ana asilimia kubwa za kufaulu majaribio hayo.
Ajib ambaye alitimkia nchini humo Jumatatu ya wiki iliyopita, anaendelea kufanya majaribio kwenye kikosi cha Golden Arrows kinachoshiriki Ligi Kuu ya Sauz na mpaka sasa tayari ameshafanya kwa siku tatu mfululizo na kikosi hicho kabla ya kupumzika jana na kuendelea tena leo.
“Nashukuru Mungu kwa siku ya kwanza niliyofanya mazoezi kocha ameonyesha kunikubali, mpaka sasa nimeshafanya mazoezi kwa siku tatu na leo (jana) tumepumzika ila kesho (leo) kama kawaida,” alisema Ajib.
Awali meneja wake, Juma Ndambile alisema kama atashindwa katika timu hiyo ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini, atakwenda kufanya majaribio Amazulu inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Afrika Kusini.
SOURCE: CHAMPIONI
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: