
Posted by On the spot Tz
11:07:00 PM
0
AZAM FC imeipiku Simba SC kwa kumaliza nafasi ya pili baada ya mechi za mwisho za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo.
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, JKT Ruvu imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba SC, mabao yake yakifungwa na Abdulrahman Mussa dakika ya kwanza na 30, wakati la Wekundu wa Msimbazi limefungwa na Nahodha Mussa Hassan Mgosi dakika ya 70.
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam pia, wenyeji Azam FC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT ya Tanga.
Ramadhani Singano ‘Messi’ alianza kuifungia Azam FC dakika ya 60 kabla ya Fully Maganga kuisawazishaia Mgambo dakika ya 72.

Kwa matokeo hayo, Azam FC inamaliza na pointi 64, ikifuatiwa na Simba SC inayomaliza na pointi 62 katika nafasi ya tatu.
Yanga SC ambayo ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu wiki mbili zilizopita, leo imemaliza kwa sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji Majimaji Uwanja wa Majimaji mjini Songea hivyo kufikisha pointi 73.
Mechi nyingine za kufunga pazia la Ligi Kuu, wenyeji Toto Africans wamefungwa 1-0 na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Coastal Union wamefungwa 2-0 na Prisons Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Mbeya City imelazimishwa sare ya 0-0 na Ndanda FC, Mtibwa Sugar wameichapa 2-0 African Sport na Kagera Sugar wameshinda 2-0 dhidi ya Mwadui FC.
Kwa matokeo hayo, timu zote za Tanga, Mgambo JKT, African Sports na Coastal Union zinaipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu, zikizipisha Ruvu Shooting, Mbao FC na African Lyon.
Mgambo JKT imemaliza na pointi 28, African Sports 26 na Coastal 22.
onthespottz.blogspot.com
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, JKT Ruvu imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba SC, mabao yake yakifungwa na Abdulrahman Mussa dakika ya kwanza na 30, wakati la Wekundu wa Msimbazi limefungwa na Nahodha Mussa Hassan Mgosi dakika ya 70.
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam pia, wenyeji Azam FC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT ya Tanga.
Ramadhani Singano ‘Messi’ alianza kuifungia Azam FC dakika ya 60 kabla ya Fully Maganga kuisawazishaia Mgambo dakika ya 72.
Kwa matokeo hayo, Azam FC inamaliza na pointi 64, ikifuatiwa na Simba SC inayomaliza na pointi 62 katika nafasi ya tatu.
Yanga SC ambayo ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu wiki mbili zilizopita, leo imemaliza kwa sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji Majimaji Uwanja wa Majimaji mjini Songea hivyo kufikisha pointi 73.
Mechi nyingine za kufunga pazia la Ligi Kuu, wenyeji Toto Africans wamefungwa 1-0 na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Coastal Union wamefungwa 2-0 na Prisons Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Mbeya City imelazimishwa sare ya 0-0 na Ndanda FC, Mtibwa Sugar wameichapa 2-0 African Sport na Kagera Sugar wameshinda 2-0 dhidi ya Mwadui FC.
Kwa matokeo hayo, timu zote za Tanga, Mgambo JKT, African Sports na Coastal Union zinaipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu, zikizipisha Ruvu Shooting, Mbao FC na African Lyon.
Mgambo JKT imemaliza na pointi 28, African Sports 26 na Coastal 22.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: