Posted by On the spot Tz
8:53:00 AM
0
YANGA SC imeondoka asubuhi ya leo kwa ndege kwenda Mwanza kwa ajili ya mechi zake mbili mfululizo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Kanda ya Ziwa.
Baada ya jana kuendeleza desturi ya ushindi katika ligi hiyo kwa kuifunga Mgambo JKT 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga inatarajiwa kucheza na Toto Africans Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Na baada ya hapo, mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu, Mei 3 watakuwa Uwanja wa Kambarage, Shinyanga kumenyana na wenyeji Stand United katika mchezo mwingine wa ligi hiyo.
Baada ya mchezo huo, Yanga itarejea Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo wake wa mchujo wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Sagrada Esperanca ya Angola Mei 8, Uwanja wa Taifa.
Baada ya mchezo huo, Ratiba ya Ligi Kuu inawapeleka Yanga Mbeya kumenyana na wenyeji Mbeya City Mei 10, mchezo ambao unaweza kuahirishwa pamoja na ule wa Mei 15 dhidi ya Ndanda FC mjini Mtwara kutokana na Yanga kuwa na mchezo wa marudiani na Esperanca Aprili 17 au 18 Angola.
Kuna uwezekano Yanga ikacheza mechi zake tatu za mwisho za Ligi Kuu mfululizo dhidi ya Mbeya City, Ndanda na Majimaji uliopangwa kuchezwa Mei 21, Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Kwa ujumla Ligi Kuu itaendelea mwishoni mwa wiki, Jumamosi mbali na Toto na Yanga, African Sports watamenyana na Coastal Union katika mechi ya mahasimu wa Jiji la Tanga, Uwanja wa Mkwakwani, Mwadui FC watamenyana na Stand United katika mechi ya mahasimu wa Shinyanga Uwanja wa Mwadui Complex, Mtibwa Sugar na Mbeya City Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro na Prisons watakuwa wenyeji wa JKT Ruvu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Jumapili kutakuwa na mchezo mtamu zaidi baina ya Simba SC na Azam FC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
onthespottz.blogspot.com
Baada ya jana kuendeleza desturi ya ushindi katika ligi hiyo kwa kuifunga Mgambo JKT 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga inatarajiwa kucheza na Toto Africans Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Na baada ya hapo, mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu, Mei 3 watakuwa Uwanja wa Kambarage, Shinyanga kumenyana na wenyeji Stand United katika mchezo mwingine wa ligi hiyo.
Baada ya mchezo huo, Yanga itarejea Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo wake wa mchujo wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Sagrada Esperanca ya Angola Mei 8, Uwanja wa Taifa.
![]() |
Yanga walipokuwa kwenye ndege asubuhi ya leo kwa safari ya Mwanza |
Kuna uwezekano Yanga ikacheza mechi zake tatu za mwisho za Ligi Kuu mfululizo dhidi ya Mbeya City, Ndanda na Majimaji uliopangwa kuchezwa Mei 21, Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Kwa ujumla Ligi Kuu itaendelea mwishoni mwa wiki, Jumamosi mbali na Toto na Yanga, African Sports watamenyana na Coastal Union katika mechi ya mahasimu wa Jiji la Tanga, Uwanja wa Mkwakwani, Mwadui FC watamenyana na Stand United katika mechi ya mahasimu wa Shinyanga Uwanja wa Mwadui Complex, Mtibwa Sugar na Mbeya City Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro na Prisons watakuwa wenyeji wa JKT Ruvu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Jumapili kutakuwa na mchezo mtamu zaidi baina ya Simba SC na Azam FC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: